بسم الله الرحمن الرحيم


بسم الله الرحمن الرحيم

UDOMSA.

Saturday 8 October 2011

TUWEKE MAZINGATIO

Bismillah.
Assalamu Alaiekum Warahmatullahi Wabarakaatuh.

Ilitokezea Siku Mmoja Katika Waja Wa Mwenyezi Mungu. Huyu Mja Alikuwa Ameghafilika Ulimwenguni. Siku Mmoja Alirejea Nyumbani Mchana Na Kula Chakula Cha Mjana Na Kwenda Kulala .

Ghafla Katika Usingi Wake Aliona Mke Wake Anakuja Kumuamsha Na Alipofika Tu Akawa Anamuamsha Mume Wangu Amka Magharibi Imekaribia. Na Yule Mke Akaona Bwana Haamki Ikiwa Anamtikisa Kila Upande Bado Haamki. Na Yule Mume Anaona Kila Kitu Atachofanyiwa Mke Wake Na Alikuwa Anamjibu Mimi Nimeshaamka Usinitikise Mimi Niko Macho Mbona Unanitikisa. Na Mke Bado Anamuona Mumewe Amelala Tu Ikawa Mke Anajaribu Kutikisa Kichwa Bado Haamki Mke Akaaza Kulia.

Na Yule Mume Anamwambia Usilie Mimi Nikomacho Mbona Unalia Mke Alipoona Mumewe Yupo Katika Hali Ilie Alikwenda Kuwaita Kaka Zake Na Dada Zake Walipofika Na Wawoo Walijaribu Kumwita Wapi Kimwa. Na Wakati Huwo Yeye Anawaambia Mimi Nimeshaamka Vipi Nyinyi Munaanza Kulia Musilie Mimi Nimzima. Na Wale Kaka Na Dada Wakaamuwa Kumwita Daktari Ili Aje Kumtizama Vipi Mambo Haya.
Na Yule Mume Anasema Huku Amehamaki Na Wawoo Vipi Nyinyi Munalia Na Sasa munataka Kumwita Daktari Mimi Mzima Hapa Lakini Nyinyi Muna Akili Au Vipi. Daktari Alifika Na Kumtizama Yule Mume Na Alisema Huyu Ameshakufa Tena Kwa Muda Sasa. Na Yeye Anasema Aee Nyinyi Mimi Ni Mzima Vipi Nyinyi Muna Akili Lakini.

Wakafika Watu Wapale Mtaani Na Mshekhe Wakaanza Kumvua Nguwo Iliwakamuoshe. Walipoanza Tu Kumgusa Na Yeye Anasema Vipi Nyinyi Nyote Akili Zenu Ziko Sawa Mimi Ni Mzima Munanivuwa Nguwo Zangu Vipi Nyinyi Munanichukuwa Nakuniosha Kama Maiti Mimi Mzima Niwacheni Niwacheni Niwacheni. Watu Waliendelea Kumuosha Na Kuvisha Sanda Na Kumtia Katika Jeneza Na Yeye Anapinga Kelele Tu Huku. Na Walimpeleka Kumsalia Na Kumchukuwa Mpaka Kaburini. Bado Yeye Anasema Musinitie Kaburini Mimi Ni Mzima.

Na Watu Walimtia Kaburini Na Kufukia Na Yeye Anawaona Kila Mmoja Waoo Anasema Nyinyi Vipi Munanifukia Na Mimi Niko Haii.Na Watu Wakafukia Kaburi Na Kumuombea Duaa Na Kuondoka Kaburini.

Sasa Yeye Anaona Kiza Tuu Kwenye Kaburi Haoni Kitu Chochote Ghafla Anaona Watu Wa Wili Moja Kasimama Katika Kichwa Chake Na Moja Miguuni Mwake. Na Yule Aliesimama Katika Miguu Yake Akawa Anamuuliza Nani Mungu Wako Wewe. Na Yeye Ikawa Anajaribu Kujibu Lakini Anashindwa Kujibu Kujibu Kila Akijaribu Anashindwa Na Huku Anaulizwa. Sasa Yule Aliye Simama Kichwani Kwake Akamuuliza Suala La Pili Nani Mtume Wako Akawa Anajaribu Kujibu Ikawa Anashindwa Alimpinga Zaruba Mmoja Tu Na Kwa Ghafla Alizinduka Katika Usingizi Wake.

Kijasho Kinamtoka Alisema Mambo Makubwa Alikwenda Kutia Uzu Na Kuanza Kusali Na Kuomba Msamaha Kwa Makosa Yake Yote. Tokea Siku Hiio Yeye Sasa Ni Mtu Wa Dini Sana Mwenye Kushikamana Nyendo Zote Alizoamrishwa Na Mwenyezi Mungu Na Mtume Wake Muhammad S.A.W.

Waislamu Jee Sisi Vipi Hapa.

Shukran

Wenu Mwenye Kukutakieni Maisha Ya Salama Katika Dunia Na Akhera.

Friday 29 July 2011

USHAURI WA BURE: LEO NA KESHO.

USHAURI WA BURE: LEO NA KESHO.
Usisahau kutenga muda wako kwa ajili ya: …………
Usisahau kutenga muda wako kwa ajili ya kuisoma dini yako.
Usisahau kutenga muda wako kwa ajili ya kuisoma Quran na Maana yake.
Usisahau kutenga muda wako kwa ajili ya kutafuta sadaka ya kujitolea kwa ajili ya uislamu iwe muda, hali na mali.
Usisahau kutenga muda wako kwa ajili ya familia yako kuzungumza nayo mambo ya dini.
Usisahau kutenga muda wako kwa ajili ya kutembelea ndugu jamaa na marafiki.
Usisahau kutenga muda wako kwa ajili ya mkeo kama umeoa na mumeo kama umeolewa.
Usisahau kutenga muda wako kwa ajili ya kumfikiria Allah (sw) na maneno yake na makatazo yake,
Usisahau kutenga muda wako kwa ajili ya kuzifikiria neema na rehma alizokuneemesha mola wako.
Usisahau kutenga muda wako kwa ajili ya kujiombea dua na usitegemee dua za misikitini na mikusanyiko.
Usisahau kutenga muda wako kwa ajili ya kuiendea riziki ya Allah aliokupangia na ukinai na kuridhika nayo.
Usisahau kutenga muda wako kwa ajili ya kuongeza ujuzi juu ya Elimu yako ya mazingira na jamii ikuzungukayo .
Usisahau kutenga muda wako kwa ajili ya kuipata na kuitafuta elimu juu ya mwili wako na maumbile yako, kuepuka maradhi na madhara juu yake.
Usisahau kutenga muda wako kwa ajili ya kujishughulisha na hidma mbalimbali kwa ajili yako, uislamu na jamii yako kwa ujumla.
Usisahau kutenga muda wako kwa ajili ya kupumzika baada ya uchovu wa shughuli, mizunguko na fikra nzito.
Usisahau kutenga muda wako kwa ajili ya kuwakumbusha watu wako na wakaribu wako juu ya haya.
Ushauri huu utaendelea inshaalah, na mnaalikwa katika muendelezo huu kwa ajili ya kuusiana.
MUHIMU KUZINGATIA HAYA KWANI UJUMBE USHAWAFIKIA
WABILLAH TAWFIQ.

Saturday 9 July 2011

SALAMU ZA KUWAAGA NDUGU ZETU-UDOMSA.

zwani.com myspace graphic comments
Twitter Backgrounds

Kila shukrani zimfikie Mola mlezi wetu na rehma na amani zimshukie Muhammad(saw),
Napenda kuchukua fursa hii kuwaatumia salamu za kuagana rasmi, kwa kutokuwepo pamoja tena katika chuo chetu hiki cha Dodoma almaaruf UDOM,sie ndugu zenu wa mwaka wa tatu tunakuageni ila tunakuachieni ujumbe muhimu sana na ujumbe huu pia kwetu tunaoondoka unatufaa sana, mie SULEIMAN ABDALLAH nimeuchagua kwa ujumla wa uzito wake kuwafikishia woote kwa maana ya wanaoondoka na wanobaki: UJUMBE wenyewe ni huu, kuwa
zwani.com myspace graphic comments
Twitter Backgrounds

PIA nawasisitiza kuwa;
zwani.com myspace graphic comments
Twitter Backgrounds

KWA SIE TUONDOKAO, UJUMBE.
Tunaoondoka tukaisimamaishe dini, hasa katika jitihada ndogo ya elimu tulioipata tunuie kwenda itumia vema ili jamii ya kiislamu na hata wasio ikanufaike nayo, tuonekane waislamu waliooelimika kwa kuyajua mazingira kutokana na level tuliofika, na sikutengana na uislamu na waislamu, swala zikaendelee mshikamano na jitihada za pamoja kama tulivyokuwa chuoni, wakina dada stara ikadumishwe na tuliokuwa hatuvai tukaanze kuvaa na kuonesha twaa ya amri ya Allah na mtume wetu, kwani hatujui lini tutarejea kwa mola.
Tukadumishe,kutenga muda na kuanzisha jitihada ya kuwa na elimu sahihi juu ya Uislamu na kuwahimiza ahali zetu juu ya msingi huu na kuifanyia kazi elimu hiyo kwani jamii yetu ina uchache na ukosefu mkubwa wa elimu sahihi kiasi makosa mengi juu ya dini tunayaona yakawaida.
NAWAAMBIA,
zwani.com myspace graphic comments
Twitter Backgrounds

NANYI MNAOBAKI PIA NAWAOMBEA DUA,
zwani.com myspace graphic comments
Twitter Backgrounds
zwani.com myspace graphic comments
Twitter Backgrounds

NINAMATUMAINI MAKUBWA KWA HATUA TULIYOFIKIA KATIKA PROGRAM ZETU NASEMA
zwani.com myspace graphic comments
Twitter Backgrounds

TUZIDI KUFANYA JUHUDI KATIKA HARAKATI ZAIDI KUIJENGA UDOMSA YENYE NGUVU YA UISLAMU KAMA VIJANA WAKIISLAMU,TUSEMENI,
zwani.com myspace graphic comments
Twitter Backgrounds

KWA KUMALIZIA SALAMU ZIMFIKIE MUHAMMAD, ALIYETUFUNDISHA UMOJA KAMA ALIVYOTUAMRISHA ALLAH SOTE TUMSIFU MTUME NA TUMWOMBEE MTUME WETU KWA KUMWAMBIA YAA MUHAMMAD
zwani.com myspace graphic comments
Twitter Backgrounds

NAWAAGA UDOMSA WOTE EX-UDOMSA,PRE-EX-UDOMSA NA UDOMSA WOOOOOOOOOOTE.
YOU HAVE TO FEE THE
zwani.com myspace graphic comments
Twitter Backgrounds

AS IAM
zwani.com myspace graphic comments
Twitter Backgrounds

Thursday 23 June 2011

THE MESSAGE FROM MUDIR

Bismillah.
this is the message from MUSSA SULEIMAN MUDIR OF UDOMSA. 2011/12
A, ALYKUM.
WOSIA WANGU KWENU TAFUTENI/WAKUBALINI WACHUMBA WENU ILACHUNGENI WASIKUTOENI KATIKA DINI SAHIHI YA UISLAMU, KWANI ALLAH (SW ASEMA KARIKA QURANI : "ATAKAYE JIFANYIA DINI ISIYOKUWA YA UISLAMU, MTU HUYO HATOKUBALIWA NA ATAKUWA NI MIONGONI MWA WENYE HASARA" HASWA KATIKA MAISHA YA AKHERA. MWISHO WA KUNUKUU.

Friday 10 June 2011

GRADUATION GREETINGS

glitter graphics
Glitter Graphics, Graduation Glitter Graphics
Not everyone is a graduate!
You're already lucky, make the most out of it!
All the best for a bright future ahead of you!
May you emerge a winner in this rat race that life offers us!
Happy Graduation!

It's time to make mistakes. It's time to then learn from them. It's time to take the wrong decisions and then keep correcting them till you're finally right. All of this so that next time when people ask you what you really want to do in life; you won't have to think, you'll just know it! Happy Graduation. May you have a successful life!

You have achieved a great success. You serious efforts have paid off and you deserve every bit of it. Congratulations and I bless you with my best wishes for you future. May God always take your care.

You are brilliant, able and ambitious. You shall always walk the glory road. Happy Graduation. I bless you with all that you need to earn many more achievements and feats in life ahead.

You dreamt, you believed, you strived and you achieved. You are an inspiration to all of us. Well done. Congratulations on your Graduation.

With a successful graduation, comes bigger challenges and obstacles in life. Tackle them out for your glory with the same zeal and vigor. Well done!

Many dream, some try, but only a few achieve. You are an achiever. You have made us all proud, keep up the good work. Congratulations on your graduation.

Monday 9 May 2011

MAKOSA YA MSINGI YALIYOMO NDANI YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KWA MTAZAMO WA UISLAMU

MAKOSA YA MSINGI YALIYOMO NDANI YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KWA MTAZAMO WA UISLAMU

Utangulizi wa muwasilishaji-Suleiman Abdallah

إن الحمد لله نحمده ونستعينه ونستغفره ، ونعوذ به تعالي من شرور أنفسنا وسيئات أعمالنا إنه من يهدِ الله فلا مضل له ومن يضلل فلا هادي له ، وأشهد أن لا إله إلا الله وحدة لا شريك له وأشهد أن محمداً عبده ورسوله ، (يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ اتَّقُواْ اللّهَ حَقَّ تُقَاتِهِ وَلاَ تَمُوتُنَّ إِلاَّ وَأَنتُم مُّسْلِمُونَ)( يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُواْ رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُم مِّن نَّفْسٍ وَاحِدَةٍ وَخَلَقَ مِنْهَا زَوْجَهَا وَبَثَّ مِنْهُمَا رِجَالاً كَثِيرًا وَنِسَاء وَاتَّقُواْ اللّهَ الَّذِي تَسَاءلُونَ بِهِ وَالأَرْحَامَ إِنَّ اللّهَ كَانَ عَلَيْكُمْ رَقِيبًا) (يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّهَ وَقُولُوا قَوْلًا سَدِيدًا * يُصْلِحْ لَكُمْ أَعْمَالَكُمْ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَمَن يُطِعْ اللَّهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ فَازَ فَوْزًا عَظِيمًا) أما بعد ، فإن خير الحديث كتاب الله ، وخير الهدي هديُ محمد صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ، وشر الأمور محدثاتها ، وكل محدثة بدعة ، وكل بدعة ضلالة ، وكل ضلالة في النار ، وبعد :

Sifa zote njema anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) na Rehema na Amani zimshukie Mtume wetu Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam) na Radhi za Mola ziwafikie Maswahaba zake wote Kiramu na kila mwenye kufuata nyayo zao mpaka siku ya Qiyaamah.
Makala haya yamekusanywa na Shaykh Salim ‘Abdur-Rahiym Barahiyan, (L.L.B. Shari’ah, L.L.M. Shari’ah and Law)na kutolewa katika blog hii na Seleman Abdallah,(BA.PPM&CD) University of Dodoma,UDOMSA.Ndugu zangu tuyasome na tuyazingatie na tuyachukulie hatua zaidi kiutekelezaji kama waislamu hasa wasomi wenzangu wa chuo kikuu.Ufuatao ni utangulizi kama nilivyo unukuu katika kitabu cha shekh.

UTANGULIZI
Kitabu ”MAKOSA YA MSINGI YALIYOMO NDANI YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KWA MTAZAMO WA UISLAMU” ni mkusanyiko wa Maudhui mbali mbali zilizotolewa na wahadhiri na wasemaji mbali mbali katika semina maalumu juu ya maudhui hiyo hapo juu iliyokusanya wanachuoni, wanasheria, walinganiaji na wasomi mbali mbali waliojikusanya katika Ukumbi wa Chuo cha Wasichana cha UMMU SALAMAH, mnamo tarehe 25 Swafar 1432 H sawa na 30 Januari 2011 M, lengo la semina hiyo lilikuwa ni kutafakari maneno ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuwataka wananchi wa Tanzania wakiwemo wanadini kuchangia maoni katika mchakato mzima wa kutungwa upya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Semina hiyo iliyoongozwa na mwenyekiti Shaykh ‘Alliy Adamu ‘Alliy kutoka Msumbiji ilitoa mapendekezo kwamba katika hatua ya awali iko haja ya kueneza yaliyopatikana katika semina hiyo kwa njia ya makongamano mengine katika kiwango cha wilaya, mikoa na Kitaifa, pia kwa njia ya mihadhara mbali mbali, khutba za ijumaa na kwa kutumia vyombo vya habari, Magazeti, Redio, Televisheni, na Makala mbali mbali.

Juhudi hii ni katika kutekeleza agizo hilo ambalo tunaamini litaleta mwamko mpya hasa kwa Waislam kuijua hali waliyo nayo kwa sasa na wanatakiwa wafanye nini.
Na kuwasaidia wale watakaoshiriki katika kutoa maoni kwenye kamati ya kuratibu maoni ya uandishi wa katiba mpya.


Shukrani

Ningependa kuchukua fursa hii kutoa shukrani za dhati kwa wale wote waliochangia mada hii hadi kupatikana kwa maandiko haya katika umbo la kitabu. Mola Ajaalie Juhudi zao hizi ziwe katika Mizani ya Matendo yao mema siku ya Qiyaamah.

Mkusanyaji:
Shaykh Salim ‘Abdur-Rahiym Barahiyan, (L.L.B. Shari’ah, L.L.M. Shari’ah and Law)
P. O.BOX 1542,
TANGA


Makosa Ya Msingi Yaliyomo Ndani Ya Katiba Ya Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Kwa Mtazamo Wa Uislamu



SURA YA KWANZA



Kwa nini Mada hii?
Tuna sababu zifuatazo zinazotufanya tuzungumzie mada hii:

1. Ni katika kulingania dini yetu kwa Jihadi ya hoja na kuzuia Munkari (Maovu).

﴿فَلَا تُطِعِ الْكَافِرِينَ وَجَاهِدْهُمْ بِهِ جِهَادًا كَبِيرًا﴾(الفرقان:٥٢ قال تعالى:

Amesema Allaah:
“Na wala usiwatii Makafiri na pigana nao Jihadi ya hoja ya (Quraan) Jihadi kubwa”. (Surat AlFurqaan: 52).

وقال تعالى:﴿ قُلْ هَذِهِ سَبِيلِي أَدْعُو إِلَى اللَّهِ عَلَى بَصِيرَةٍ أَنَا وَمَنِ اتَّبَعَنِي وَسُبْحَانَ اللَّهِ وَمَا أَنَا مِنَ الْمُشْرِكِينَ ﴾(يوسف:١٠٨).

Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Sema hii ndio njia yangu nalingania kwa Allaah kwa ujuzi mimi na yule aliyenifuata na Ametakasika Allaah na kila upungufu nami si katika washirikina”
(Surat Yuusuf: 108).

وقال صلى الله عليه وسلم:(من رأى منكم منكرا فليغيره بيده فإن لم يستطع فبلسانه فإن لم يستطع فبقلبه وذلك أضعف الإيمان)رواه مسلم.

Amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam):
“Atakaeona miongoni mwenu ovu lolote aliondoe kwa mkono yake, na kama hataweza basi na kwa ulimi wake na kama hataweza basi na aliondoe kwa moyo wake (alichukie) na hali hii (kulichukia kwa moyo) ni udhaifu mkubwa wa imani” (Imepokewa na Imaam Muslim).

عن النعمان بن بشير رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال:(مثل القائم في حدود الله والواقع فيها كمثل قوم استهموا على السفينة فصار بعضهم أعلاها وبعضهم أسفلها وكان الذين في أسفلها إذا استقوا الماء مروا على من فوقهم فقالوا لو أنا خرقنا في نصيبنا خرقا ولم نأذي من فوقنا،فإن تركوهم وما أرادواهلكوا جميعا وإن أخذوا على أيديهم نجوا ونجوا جميعا).رواه البخاري.

Toka kwa Nu”umaan bin Bashiyr (Radhiya Allaahu ‘anhu) amepokea toka kwa Nabii (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam) akisema:
“Mfano wa yule aliesimama katika mipaka ya Allaah na yule alievuka mipaka yake ni mfano wa watu walioingia kwenye Safina kwa kupiga kura na wakawa miongoni mwao juu ya ile Safina na wengine chini (inaashiria ukubwa wa hiyo Safina) ikawa wale waliokuwa chini wakitaka maji huyafuata kwa kupitia kwa wale wa juu, wakasema (kwa kushauriana): kama tungetoboa hukuhuku chini tungeyapata maji bila ya kuwaudhi wenzetu walio juu, kama wataachwa na matakwa yao hayo wataangamia wote na kama wakizuiwa wataokoka wote).”
(Imepokewa na Imaam Al-Bukhaariy).

قال الله تعالى:﴿ كُنْتُمْ خَيْرَ أُمَّةٍ أُخْرِجَتْ لِلنَّاسِ تَأْمُرُونَ بِالْمَعْرُوفِ وَتَنْهَوْنَ عَنِ الْمُنْكَرِ وَتُؤْمِنُونَ بِاللَّهِ)( آل عمران:١١٠)
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Mmekuwa Umma bora utokanao na watu mnaamrishana mema na mnakatazana mabaya na mnamwamini Allaah” (Surat Al-‘Imraan: 110).


2. Ni haki ya Kikatiba kwa kila Raia:

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Tanzania 18(1):
“Bila kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa”


3. Ni wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa Raia wa nchi hii kuchangia maoni katika mchakato wa kuandikwa upya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania:

Katika Gazeti la MWANANCHI la Jumamosi tarehe 1 Januari 2011:
“Rais Jakaya Kikwete ametangaza kuanza mchakato wa kuandikwa katiba Mpya.Katika salamu zake za mwaka mpya kwa Taifa jana, Rais Kikwete alisema: “Nimeamua kuunda Tume Maalumu ya Katiba yaani Constitutional Review Commision. Tume hiyo itakayoongozwa na Mwanasheria aliyebobea, itakuwa na wajumbe wanaowakilisha makundi mbali mbali kutoka jamii yetu kutoka pande mbili za Muungano, alisema jukumu la msingi la Tume hiyo litakuwa ni kuongoza na kuratibu mchakato utakaowashirikisha wanasiasa, wafanyabiashara, asasi za kiraia, mashirika ya dini, wanataaluma na makundi mbali mbali ya watu wote, katika kutoa maoni wayatakayo kuhusu katiba ya nchi yao.”


4. Ni wajibu wetu kutoa Nasaha:

قال تعالى:﴿ وَإِنْ أَحَدٌ مِنَ الْمُشْرِكِينَ اسْتَجَارَكَ فَأَجِرْهُ حَتَّى يَسْمَعَ كَلَامَ اللَّهِ (التوبة:٦).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Kama mmoja yeyote katika washirikina atakuomba awe karibu nawe basi kuwa karibu nae ili apate kusikia maneno ya Allaah”
(Surat At-Tawbah: 6).

عن التميم الداري رضي الله عنه أن النبي صلى الله عليه وسلم قال:(الدين النصيحة.قلنا لمن يارسول الله.قال:لله ولكتابه ولرسوله ولأئمة المسلمين وعامتهم).رواه مسلم.
Imepokewa na Tamiym Ad-Daariy (Radhiya Allaahu ‘anhu),
Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam):
“(Dini ni nasaha) tukasema kwa ajili ya nani ewe mjumbe wa Mwenyezi Mungu? akasema:kwa ajili ya Allaah na Kitabu Chake na Mtume Wake na kwa viongozi wa Waislamu na watu wote)”
(Imepokewa na Imaam Muslim).

وقال صلى الله عليه وسلم:(إذا استشار أحدكم أخاه فليشر عليه).رواه ابن ماجه.
Amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam):
“Atakapotaka ushauri mmoja wenu kwa ndugu yake basi amshauri”.
(Imepokewa na Ibn Maajah).


5. Kuwatanabaisha baadhi ya masheikh ambao mara baada ya Rais kutangaza mchakato wa Katiba mpya wakakurupuka na kutoa maoni kwamba wanataka mahakama ya Qaadhi (Kadhi) na nchi kujiunga na OIC na Ijumaa iwe ni siku ya mapumziko, na wameghafilika kwamba Katiba imewanyima haki zao za msingi na kubwa kuliko mahakama ya Qaadhi na OIC na siku ya Ijumaa. Na wengine kuona bado wakati wa kutoa maoni wamewausia WaIslamu wasiseme kitu wasubiri kamati ya kukusanya maoni itakayoundwa na Mheshimiwa Rais.

SURA YA PILI

Nini Maana Ya Katiba Ya Nchi? Kwa Mtazamo Usio Wa Kidini.

Katika nchi yoyote msingi wa uendeshaji wa nchi unategemea Katiba. Katiba ni sheria kuu au sheria mama katika nchi yoyote. Sheria nyingine zote zinategemea au zinatungwa kwa mujibu wa katiba, wakati mwingine katiba hutafsiriwa kuwa ni mkataba wa kijamii kati ya watawala na wananchi (watawaliwa). Ni makubalianao ya wananchi husika juu ya ni jinsi gani taratibu za kanuni za uendeshaji wa mambo mbali mbali katika nchi yao unapaswa kuwa.
(Angalia kitabu HAKI Tolea la 5 Namba 4 Dec. 2002 Uk. 6).

Ni muafaka wa Kitaifa juu ya misingi mikuu ya kuendesha nchi.
(Maneno ya Pro.Shivji katika kongamano tarehe 15/1/2011Dar es Salaam.)


Maana ya katiba ya nchi kwa mtazamo wa Kiislamu

Sheria kuu na Sheria Mama katika nchi kwa mujibu wa Uislamu ni Qur-aan na Sunnah ya Mtume (Swalla Allaahu ‘Alayhi wa sallam).

قال تعالى:﴿ فَإِنْ تَنَازَعْتُمْ فِي شَيْءٍ فَرُدُّوهُ إِلَى اللَّهِ وَالرَّسُولِ﴾.(النساء:٥٩).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Ikiwa mkikindana (kukhitalifiana) katika jambo lolote basi lilerejesheni (jambo hilo) kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake”
(Surat An-Nisaa: 59).

قال تعالى:﴿ وَمَا كَانَ لِمُؤْمِنٍ وَلَا مُؤْمِنَةٍ إِذَا قَضَى اللَّهُ وَرَسُولُهُ أَمْرًا أَنْ يَكُونَ لَهُمُ الْخِيَرَةُ مِنْ أَمْرِهِمْ وَمَنْ يَعْصِ اللَّهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا مُبِينًا ﴾(الأحزاب:٣٦).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Na haifai kwa muumini mwanamme au mwanamke pale atakapolitolea hukumu jambo lolote Mwenyezi Mungu na Mtume wake wawe na hiari katika kulitekeleza Jambo hilo, na anae muasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake hakika amepotea upotevu wa wazi)”
(Surat Al-Ahzaab: 36).



Historia Ya Katiba Katika Nchi Zilizotawaliwa Na Makafiri

“Kwa ujumla nchi nyingi hasa zile zinazoendelea zina katiba zilizoandikwa.nyingi kati ya katiba hizo zilitungwa na kurekebishwa na watawala wa kikoloni, na nyingine zilitungwa baada ya makubaliano na tawala za kikoloni kabla ya kuondoka.Katiba hizo ni maridhiano ambayo yalilinda maslahi ya pande zote mbili:
(1)Tawala za kikoloni zilizokuwa zikiandika.
(2)Nchi iliyokuwa ikipata uhuru(Angalia Jarida la HAKI Toleo la 5 uk.7), (Angalia pia Shetani wa mwalimu uk.6):
"Katiba nyingi katika nchi zilizoendelea zina uhusiano na Katiba na Tawala za kikoloni.
Historia ya katiba hapa Tanzania pia ina uhusiano na tawala za kikoloni zilizokuwa zinatawala kabla ya uhuru".Angalia HAKI toleo la 5 uk.7(Kamati ya Msaada ya Kisheria).


Historia Ya Mabadiliko Ya Katiba Tanzania

1961Katiba ya kwanza ya uhuru iliyowekwa na waingereza (Independence Constitution).
1962Katiba ya Jamhuri (The Republic Constitution) iliitambua Tanganyika kama Jamhuri na ilipunguza madaraka ya Bunge(Imewekwa na Waingereza).
1965Iliwekwa katiba ya muda (The Interim Constitution)
1977Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilitungwa na bunge maalum (Constitutional Assembly), (wananchi hawakuhusishwa).Angalia HAKI toleo la 5 uk.10).
Pr.Issa Shirji anabainisha haya pia katika kongamano la Katiba lililoandaliwa na wanataaluma wa chuo kikuu cha Dar es Salaam, Jumamosi tarehe 15/1/2011 angalia Gazeti la MWANANCHI uk.4 tarehe 16/1/2011.


Mabadiliko Makubwa Yaliyotokea Katika Katiba

1961Katiba iliruhusu mfumo wa vyama vingi,
Vyama vifuatavyo vilisajiliwa:TANU, United Tanganyika Party(UTP), African National Congress(ANC), The Peoples Democratic Party(PDP), Peoples Convertion Party(PNP), National Enterprise Party(NEP), All Muslim Nationalist Union of Tanganyika(AMNUT), African Independence Movement(AIM).
1963Halmashauri kuu ya TANU ilipitisha maamuzi kufanya Tanganyika kuwa nchi ya chama kimoja.
1965Sheria ya chama kimoja iliingizwa kwenye Katiba.1977Haki za binaadamu ziliingizwa rasmi katika Dibaji.
1984Katika katiba ya Jamhuri haki za binaadamu ziliingizwa rasmi katika katiba.
1992Katiba iliruhusu tena mfumo wa vyama vingi kwa shinikizo la nchi za kibeberu (kikafiri).
Katika kitabu: Elimu ya Demokrasia shirikishi (Kitabu kilichotolewa na CTP Dom uk.7) chasema hivi:
"Wanasayansi wa mambo ya siasa wanaelekea kukubali kwamba demokrasia ya vyama vingi imeingizwa toka nje kwa kutokana na masharti ya kupata misaada ya fedha".


Katiba Ya Allaah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Haibadiliki

قال تعالى:﴿ وَاتْلُ مَا أُوحِيَ إِلَيْكَ مِنْ كِتَابِ رَبِّكَ لَا مُبَدِّلَ لِكَلِمَاتِهِ﴾(الكهف:٢٧).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):”Nawasomee kilichoteremshwa kwako kwa wahyi (Ufunuo) katika kitabu cha Mola wako ambacho hayabadiliki maneno yake)” (Surat Al Kahfi: 27).
قال تعالى:﴿ وَإِنَّهُ لَكِتَابٌ عَزِيزٌ. لَا يَأْتِيهِ الْبَاطِلُ مِنْ بَيْنِ يَدَيْهِ وَلَا مِنْ خَلْفِهِ تَنْزِيلٌ مِنْ حَكِيمٍ حَمِيدٍ﴾
(فصلت:٤١-٤٢)
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Na hakika hiyo (Qur-aan) ni Kitabu kitukufu, hakiingiliwi na batili yoyote mbele yake wala nyuma yake imeteremka kutoka kwa Mwenye hekima ya hali ya juu na Mwenye kushukuriwa sana)”
(Surat Fusswilat: 41- 42).






SURA YA TATU

Mambo Ya Msingi Yaliyomo Ndani Ya Katiba Yanayokwenda Kinyume Na Uislam

1. Mfumo Wa Demokrasia

Nini maana ya Democracy?
Ni neno lenye asili ya kigiriki (Demo – crates) yaani utawala wa watu.
"Ni mfumo wa kuendesha serikali ya watu iliyochaguliwa na watu kwa manufaa ya watu, madaraka na mamlaka, ya mwisho ya serikali hiyo yako mikononi mwa watu"
(Angalia Jifunze Uraia kwa shule za msingi kitabu cha nne na S. A. Numisi uk. 10).

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania, sehemu ya pili, Serikali na watu, sheria ya 1984 na.15, 16.6,
“Jamhuri ya muungano wa tanzania ni nchi inayofuata misingi ya demokrasia na haki za kijamii na kwa hiyo:
a) Wananchi ndiyo msingi wa mamlaka yote na serikali itapata madaraka na mamlaka yake kutoka kwa wananchi kwa mujibu wa katiba hii.
b) Lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi serikali itawajibika kwa wananchi”


2. Mamlaka Ya Kutunga Sheria Yako Mikononi Mwa Watu Badala Ya Allaah (Subhaanahu Wa Ta’ala)

Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kifungu 64 (1):
“Mamlaka yote ya kutunga sheria juu ya mambo yote yahusuyo Tanzania bara yatakuwa mikononi mwa bunge”

Kifungu 106 (3):
Madaraka yote ya kutunga sheria katika zanzibar katika mambo yote yasiyo mambo ya muungano yatakuwa mikononi mwa baraza la wawakilishi wa Zanzibar.


3. Mfumo Wa Kutenganisha Dini Na Mamlaka Ya Nchi (Siasa)

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania kifungu 19 (2):
“Bila kuathiri sheria zinazohusika za jamhuri ya muungano, kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari ya mtu binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuia za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi”.

Katika katiba toleo la 2005 ibara ya 3:
3 (1) “Jamhuri ya muungano ni nchi ya kidemokrasia na ya kijamaa, isiyokuwa na dini yenye kufuata mfumo wa vyama vingi vya siasa”.


4. Mfumo Wa Kufuata Siasa Ya Ujamaa Kwa Mujibu Wa Katiba Ya Jamhuri Ya Muungano

Kifungu cha 9:
“Lengo la katiba hii ni kuendesha ujenzi wa jamhuri ya muungano na serikali ya mapinduzi ya Zanzibar au wa chochote kati ya vyombo vyake na udugu wa amani kutokana na kufuata siasa ya ujamaa na kujitegemea, ambayo inasisitiza utekelezaji wa misingi ya kijamaa kwa kuzingatia mazingira yaliyomo katika jamhuri ya muungano”.


5. Mfumo Wa Kukataza Kuanzishwa Chama Cha Siasa Chenye Lengo La Kukuza Dini

Kwa mujibu wa katiba kifungu 20 (2):
“Kwa kujali masharti ya ibara ndogo (1) haitakuwa halali kwa chombo chochote cha siasa kuandikishwa ambacho kutokana na katiba au sera yake:
A) kinakusudia kukuza au kupigania maslahi ya:
I) “imani au kundi lolote la dini”.


6. Sera Ya Kulazimisha Kila Raia Kufuata Na Kutii Katiba Ya Jamhuri Na Sheria Zake Hata Kama Zinakhalifu Shari”ah Ya Allaah (Subhaanahu Wa Ta’ala)

Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri kifungu 26 (1):
“Kila mtu ana wajibu wa kufuata na kutii katiba hii na sheria za jamhuri ya muungano”.


7. Kiongozi Wa Nchi (Rais) Kupewa Madaraka Ya Kuchupa Mipaka (Udikteta)

Ka mujibu wa katiba ya jamhuri kifungu 45 (1):
“Bila ya kuathiri masharti mengineyo yaliyomo katika ibara hii, rais anaweza kutenda lolote kati ya mambo yafuatayo:
A) kutoa msamaha kwa mtu yoyote aliyepatikana na hatia mbele ya mahakama kwa kosa lolote na aweza kutoa msamaha bila masharti au kwa masharti kwa mujibu wa sheria.
B) kumwachilia kabisa au kwa muda maalumu mtu yeyote aliyehukumiwa kuadhibiwa kwa ajili ya kosa lolote ili mtu huyo asitimize kabisa adhabu hiyo wakati wa muda huo maalum.
C) kuibadilisha adhabu yoyote aliyopewa mtu yeyote kwa kosa lolote iwe adhabu tahafifu.
D) kufuta adhabu yote au sehemu ya adhabu yote”.


8. Uhuru Wa Kubadilisha Dini Anayotaka

Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri kifungu 19 (1):
“Kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo, imani na uchaguzi katika mambo ya dini, pamoja na uhuru wa mtu kubadilisha dini au imani yake”.


9. Sera Ya Kugombea Uongozi Badala Ya Kugombewa

Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri kifungu 67 (3):
“Mtu hataweza kugombea uchaguzi kuwa mbunge wa kuwakilisha jimbo la uchaguzi katika uchaguzi mkuu wowote ikiwa wakati huo yeye amesimama katika uchaguzi kugombea kiti cha Rais, wala hataweza kugombea uchaguzi kuwa mbunge katika uchaguzi mdogo wowote ikiwa yeye ni Rais”.


10. Mfumo Wa Vyama Vingi Vya Siasa

Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri kifungu 3 (1):
“Jamhuri ya muungano ni nchi ya kidemokrasia na ya kijamaa, yenye kufuata mfumo wa vyama vingi vya siasa”.


11. Kiongozi Mkuu Wa Nchi (Rais) Kuwa Juu Ya Sheria

Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri kifungu 46:
(1): wakati wote Rais atakapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa katiba hii, itakuwa ni marufuku kumshitaki au kuendesha mashtaka ya aina yoyote juu yake mahakamani kwa ajili ya kosa lolote la jinai.

(2) wakati wote Rais atakapokuwa bado ameshika madaraka yake kwa mujibu wa katiba hii, haitaruhusiwa kufungua mahakamani shauri kuhusu jambo lolote alilolitenda au alilokosea kulitenda yeye binafsi kama raia wa kawaida ama kabla au baada ya kushika madaraka ya Rais…


12. Matumizi Ya Mapambano (Jihadi) Yanakataliwa

Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri kifungu 20 (21):
“Bila ya kujali masharti ya ibara ndogo (1) haitakuwa halali kwa chombo chochote cha siasa kuandikishwa ambacho kutokana na katiba na sera zake:
(c) kinakubali na kufungamana na matumizi ya nguvu au mapambano kama njia ya kufikia malengo yake ya kisiasa”.


13. Itikadi Ya Al-Walaa Wal-Baraa (Kupenda Kwa Ajili Ya Allaah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Na Kuchukia Kwa Ajili Ya Allaah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Inavunjwa

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Haki ya Usawa, kifungu 12(4):
Ni marufuku kwa mtu yeyote kubaguliwa na mtu au mamlaka yote inayotekeleza madaraka yake chini ya sheria yoyote au katika utekelezaji wa kazi au shughuli yoyote ya mamlaka ya nchi.

Kifungu 12 (5):
Kwa madhumuni ya ufafanuzi wa masharti ya ibara hii neno “kubagua” maana yake ni kutimiza haja, haki, au mahitaji mengineyo kwa watu mbali mbali kwa kuzingatia utaifa wao, kabila, pahali walipotokea, maoni ya kisiasa, rangi, dini, jinsia au hali ya maisha kwa namna ambapo watu wa aina fulani wanafanywa au kuhesabiwa dhaifu au duni au kuwekewa vikwazo au masharti ya upingamizi ambapo watu wa aina nyingine wanatendewa auwanapewa fursa au faida iliyoko nje ya masharti au sifa za lazima isipokuwa kwamba neno “kubagua” halitafafanuliwa kwa maana ambayo “itazuia serikali kuchukua hatua za makusudi zenye lengo la kurekebisha matatizo katika jamii.

SURA YA NNE

Baadhi Ya Vipengele Na Maneno Yaliyomo Ndani Ya Katiba Vilivyopotoshwa Kwa Mtazamo Wa Uislamu


1. Neno Ibada: Limepewa Tafsiri Finyu

Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri kifungu 18 (2):
Bila kuathiri sheria zinazohusika za jamhuri ya muungano, kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada au kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari ya mtu ya binafsi na shughuli za uendeshaji wa jumuia za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.


2. Neno Halali

Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri kifungu 9:
Mamlaka ya nchi na vyombo vyake vyote vinawajibika kuelekeza sera na shughuli zake zote katika lengo la kuhakikisha:
(e)kwamba kila mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi, anafanya kazi, na kazi maana yake ni shughuli ya halali inayompatia mtu riziki yake”.


3. Neno Usawa

Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri kifungu 13(1):
WATU WOTE MBELE YA SHERIA NA WANAYO HAKI, BILA YA UBAGUZI WOWOTE, KULINDWA NA KUPATA HAKI SAWA MBELE YA SHERIA.
Vile vile kifungu 12(1):
BINAADAMU WOTE HUZALIWA HURU NA WOTE NI SAWA.


4. Neno Haki Ya Kuishi

Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri kifungu (1):
Kila mtu anayo haki ya kuwa huru na kuishi kwa uhuru.
Hii imetafsiriwa kwamba hata aliyeua asiuliwe kwa sababu ana haki ya kuishi.


5. Neno Haki Ya Kumiliki

Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri kifungu 24 (1):
“Bila kuathiri masharti ya sheria za nchi zinazohusika, kila mtu anayo haki ya kumiliki mali na haki ya hifadhi kwa mali yake aliyonayo kwa mujibu wa sheria”
Imefasiriwa kipengele hiki kwamba mtu ana haki ya kugawa urithi, atakavyo yeye maadam ni mali yake.


6. Kufutwa Adhabu Ya Viboko

Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri kifungu 136(e):
Ni marufuku kwa mtu kuteswa kinyama au kupewa adhabu zinazomtweza au kumdhalilisha.
Mahakama kuu Dodoma katika kesi ya Thomas s/o Mjengi Vrs.R, Dodoma High Court Criminal appeal Na.28/1991 hapo tarehe 23/6/1992 ilihukumiwa kuwa adhabu ya viboko na adhabu ya kima cha chini cha kifungo cha miaka 30 kwa kosa la unyang”anyi ni kinyume cha Ibara ya 13(6) (e) ya Katiba yetu.






SURA YA TANO

Mtazamo Wa Uislamu Kuhusu:

1. Mfumo Wa Democracy

Ni matunda ya mapinduzi ya Kifaransa.

Demokrasia ni ushirikina Kwa sababu inampa Mwanaadamu Mamlaka na Madaraka ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala).

Historia Ya Mapinduzi Ya Ufaransa

Kanisa la Ki-Roma lilitawala nchi za Ulaya kwa muda mrefu katika nchi za Ulaya. Kanisa lilidhulumu haki nyingi za raia wa Ulaya kwa jina la dini, hii ilipelekea kujitokeza wanaharakati kupinga dhulma hii ya kanisa, harakati hizo zilipelekea kufanyika Mapinduzi makubwa huko Ufaransa mwaka 1789 jambo ambalo limepelekea kanisa kuvuliwa madaraka ya Kisiasa na athari ya mapinduzi hayo ndiyo yaliyozusha mfumo wa:

1. Democracy: Watu ndio wenye mamlaka ya kila kitu.
2. Secularism: Kutenganisha Dini na Mamlaka ya nchi (Siasa).
Mfumo wa Demokrasia ni Ushirikina kwa sababu unampa mwanaadamu mamlaka ya Mungu.

قال تعالى:﴿ لَا تُشْرِكْ بِاللَّهِ إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ﴾ (لقمان:١٣).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Wala usimshirikishe Allaah hakika ya ushirikina ni dhulma kubwa)”
(Surat al-Luqmaan:13).

وقال تعالى: ﴿ وَلِلَّهِ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاللَّهُ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴾ (آل عمران:١٨٩)
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Ni milki ya Allaah tu vilivyomo mbinguni na Ardhini na Allaah juu ya kila kitu ni muweza.”
(Surat al-‘Imraan: 189).


2. Ni Nani Mwenye Haki Ya Kuweka Sheria?

قال تعالى: ﴿ أَلَا لَهُ الْخَلْقُ وَالْأَمْرُ﴾ (الأعراف:٥٤).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Eleweni ni miliki yake yeye tu (Allaah) kuumba na kuamrisha)”
(Surat Al-A’araaf: 54)

وقال تعالى: ﴿ إِنِ الْحُكْمُ إِلَّا لِلَّهِ أَمَرَ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا إِيَّاهُ﴾ (يوسف:٤٠).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“(Hukumu ni ya Allaah (peke yake) ameamrisha musiabudu chochote isipokuwa yeye tu)”Surat Yusuf: 40).

وقال تعالى: ﴿ اتَّخَذُوا أَحْبَارَهُمْ وَرُهْبَانَهُمْ أَرْبَابًا مِنْ دُونِ اللَّهِ وَالْمَسِيحَ ابْنَ مَرْيَمَ وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا إِلَهًا وَاحِدًا لَا إِلَهَ إِلَّا هُوَ سُبْحَانَهُ عَمَّا يُشْرِكُونَ﴾ (التوبة:٣١).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“(Wamewafanya (Mayahudi na manaswara) wanazuoni wao na watawa wao na ‘Iysa mtoto wa Maryamu kuwa ni miungu kinyume na Allaah, na hali ya kuwa hawakuamrishwa isipokuwa wamwabudu Mungu mmoja hakuna mungu mwingine anaepasa kuabudiwa isipokuwa Yeye tu utakasifu ni Wake na kila kile ambacho wanachomshirikisha nacho)”
(Surat At-Tawbah: 31)

Katika Aya hii, Mayahudi na Manaswara wamelaumiwa kwa kuwageuza wanachuoni wao na watawa wao kuwa ni Miungu kwa sababu waliwahalalishia yaliyoharamishwa na Mola na wao wakawatii na waliwaharamishia yaliyoharamishwa na Mola na wao wakawatii. Kazi ya kuweka Sheria ni ya Allaah tu peke yake sio ya Mtu wala Bunge.

وقال تعالى: ﴿ أَفَحُكْمَ الْجَاهِلِيَّةِ يَبْغُونَ وَمَنْ أَحْسَنُ مِنَ اللَّهِ حُكْمًا لِقَوْمٍ يُوقِنُونَ﴾ (المائدة:٥٠).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Hivi wanataka wahukumiwe na hukumu ya Kijahili?! Na ni Nani (hakuna) mwenye hukumu ya sawa (zaidi ya Allaah) kwa watu wenye kuyakinisha?”
(Surat Al-Maaidah: 50).


Sheria Ya Ndoa Ya 1971 Iliyotungwa Na Binaadam Ilivyokiuka Shari’ah Za Allaah (Subhaanahu Wa Ta’ala) Za Ndoa

Kifungu 160:
Mwanamme na mwanamke wakiishi pamoja kwa muda wa miaka 2 mfululizo huweza kuchukuliwa ni mke na mme mbele ya sheria japokuwa hawakuwahi kufunga ndoa.
Ndoa hii haitambuliwi katika Uislam bali inahesabiwa ni uzinifu.

قال تعالى: ﴿ وَلَا تَقْرَبُوا الزِّنَا إِنَّهُ كَانَ فَاحِشَةً وَسَاءَ سَبِيلًا ﴾ (الإسراء:٣٢).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Musiikaribie zinaa hakika hiyo (zinaa) ni uchafu na njia mbaya”
(Surat Al-Israa 32).

Kifungu cha 18 (1):
Iwapo mwanamme na mwanamke wanaotaka kuoana, itawabidi kutoa taarifa ya nia yao ya kuoana kwa msajili au ofisa wa usajilishaji kwa siku 21 kwa uchache, kabla ya siku wanayotaka kuoana kufika.

Kifungu Cha 114:
Inakatazwa katika kifungu hiki mtu kuoa au kuolewa na mzazi wake, mtoto au mjukuu wake, kama ni dada yake, mama au shangazi au baba na mjomba wake, baba au mama wa kambo na mwanae aliyemfanya mwanae (adopted child).
Katika Uislam anaelelewa anaweza kuolewa na mwenye kumlea.


Sheria ya Kiislamu Haiwezi Kuvunja Sheria ya Ndoa 1971

Kwa Mujibu wa Sheria iliyotungwa na Binaadam:
(Cap. (Kiambatanisho 453: The rules of cust Omary law and the rules of Islamic law shall not apply in regard to any matter provided for in the law of Marriage Act 1971 (Angalia Sheria ya Kiislamu ya Mirathi na Wasia – na Mahmoud A. Sameja) uk. 37

Paragraph 1 of Government Notice No.196 of 1971 made under Sect.102 of The Law of Marriage Act Categorically states that:
The above Boards (Marriage Conciliation Boards) must comply with the provisions of the law of marriage Act and any other provisions hereunder.
(Angalia Bakwata and the Administration of Islamic law: Problems: A case study of DSM by Mohammad Awadh).


Tafsiri (Isiyo Rasmi):
Kanuni za sheria za kimila na kanuni za sheria ya Kiislam haitoruhusiwa kutumika katika suala lolote linalohusiana na sheria za Ndoa ya mwaka 1971.
((Angalia Sheria ya Kiislamu ya Mirathi na Wasia – na Mahmoud A. Sameja) UK.37).

Kipengele cha 1 cha Tangazo la serikali namba 196 ya 1971 iliyotungwa chini ya kifungu cha 102 cha sheria ya Ndoa katika mfululizo inayosema kwamba:
Kamati tajwa hapo juu (Kamati za usuluhishi wa Ndoa) lazima zifuate vifungu vya sheria ya Ndoa na vipengele vingine.
(Angalia Bakwata and the Administration of Islamic law: Problems: A case study of DSM by Mohammad Awadh).

Kifungu 153 (1):
Mtu yeyote ambaye ni mmoja wa wafunga ndoa au anaeshiriki kwenye shughuli ya ndoa iwapo:
(a) mke anaekusudiwa yuko chini ya umri wa miaka 18 na idhini ya ndoa kama inavyotakiwa na fungu la 17 haikutolewa au;
(b) taarifa ya nia ya kufunga ndoa, kama inavyotakiwa na fungu la 18, haikutolewa.
Basi mtu huyu atakuwa ni mkosa na atakapoonekana kuwa ana hatia astahiki kifungo kwa muda usiozidi miezi sita.

Kwa Makusudio ya fungu la 148 mpaka 155 kushiriki kwa shughuli ya ndoa yake:
a. Kufungisha ndoa hiyo, au
b. Kutoa idhini katika ndoa hiyo
c. Kuwa shahidi wa ndoa hiyo

Wakati sheria hizi zinatungwa 1971 BAKWATA ilishindwa kutetea Uislam na moja ya malengo ya kuundwa kwake yamebainishwa ndani ya katiba yao:
MADHUMUNI 9,
“Madhumuni ya Baraza Kuu la waislam Tanzania yatakuwa haya yafuatayo:
2. kusimamia na kutetea haki za Msingi za Waislam nchini na kukemea mambo yanayoleta kero kwa waislam”

Je Sheria ya Ndoa ya Kiislam sio katika haki za kimsingi za waislam? Mbona BAKWATA imekaa kimya juu ya hili?


3. Mfumo Wa Kutenganisha Dini Na Dola (Mamlaka/Utawala) Wa Nchi

Uislam hautenganishi mamlaka ya nchi (siasa) na dini kwani Dini inatuongoza waislam katika kila kipengele cha maisha ibada, jamii, siasa uchumi n.k.

قال تعالى: ﴿قُلْ إِنَّ صَلَاتِي وَنُسُكِي وَمَحْيَايَ وَمَمَاتِي لِلَّهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ﴾ (الأنعام:١٦٢).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Waambie Swalah yangu na ibada zangu (kuchinja kwangu) na uhai wangu na kifo changu ni kwa ajili ya Allaah Mola wa viumbe wote”
(Surat Al-An’aam: 162).

Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam) na Makhalifa wake walikuwa ni viongozi wa mamlaka ya Dini na Nchi (siasa).

Kutekeleza Sheria za Jinai ni katika sehemu ya Dini

قال تعالى: ﴿ الزَّانِيَةُ وَالزَّانِي فَاجْلِدُوا كُلَّ وَاحِدٍ مِنْهُمَا مِئَةَ جَلْدَةٍ وَلَا تَأْخُذْكُمْ بِهِمَا رَأْفَةٌ فِي دِينِ اللَّهِ إِنْ كُنْتُمْ تُؤْمِنُونَ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الْآَخِرِ﴾ (النور:٢).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Mzinifu mwanamke na mzinifu mwanaume wapigeni kila mmoja wao mijeledi mia moja wala isiwachukueni huruma katika kutekeleza Dini ya Mwenyezi Mungu ikiwa (kweli) mnamuamini Allaah na siku ya mwisho”
(Surat An-Nuur: 2).

Kutekeleza sheria za jinai ni sehemu ya dini na imani, hii ni hoja dhidi ya wale waislam wanaotaka u-Qaadhi wa ndoa, talaka, mirathi wakfu, malezi na wasia tu na sio u-Qaadhi wa shari’ah zote.



Kiongozi Wa Nchi Ya Kiislam Ni Kiongozi Wa Kisiasa Pia

وقال أبوالحسن الماوردي الشافعي رحمه الله (ﺕ٤٣٠):الإمامة موضوعة الخلافة النبوة في حراسة الدين وسياسة الدنيا وعقدها لمن يقوم بها في الأمة واجب بالإجماع(الأحكام السلطانية\ص ٥).
“Na amesema Abu Al-Hasan Al-Mawardiy mfuasi wa Imaam Ash-Shafi’iy (aliekufa mwaka 430 H.), Uongozi ni shemu ya Ukhalifa wa utume Katika kulinda Dini na siasa ya dunia na kuusimamisha kwa yule anaesimamia hilo katika umma ni wajibu kwa makubaliano ya wanazuoni.
(Kitabu Al-Ahkaam As-Sultaaniyyah, uk. 2).

قال ابن تيمية رحمه الله:(فالواجب اتخاذ الإمارة دينا وقربا يتقرب بها إلى الله فإن التقرب إليه فيها بطاعته وطاعة رسوله من أفضل القربات:(السياسة الشرعية\١١٩).
Amesema Shaykh wa Uislamu Ibnu Taymiyyah (Allaah Amrehemu):
‘‘Basi ni wajibu kuweka uongozi kwa ajili ya Dini na kujikurubisha kwa Allaah hakika kujikurubisha kwa Allaah kwa kumtii na kumtii Mtume wake ni katika vikurubisho (Ibada) bora.’’
(Kitabu As-Siyaasatu Ash-Shar’iyah, uk, 119).


Viongozi Wa Majimbo Walikuwa Wanasiasa Zama Za Makhalifa

ولى الفاروق عمار بن ياسر على الكوفة،ثم كتب أهلها شكوى ضد عمار بأنه ليس بأمير ولا يحتمل،فاستدعى عمر رضي الله عنه عمار بن ياسر رضي الله عنه فأقبل ومعه جمع من أهل الكوفة فسألهم عمر فقالوا:هو والله غير كاف ولا يجزأ ولا عالم بالسياسة ولا يدري علام استعملته.فسأله عمر بحضورهم عن أمور ولايته ممتحنا إياه لمعرفة مدى خبرته في الحكم.فلم يجب بما يرضى عمر فعزله.(تاريخ الطبرى ج\٤،ص ١٦٢).
(Al Faruuq ‘Umar Ibn Al Khattwaab alimpa utawala ‘Ammaar Bin Yaasir huko Kuuufah, kisha watu wake wakamshitaki kwamba si kiongozi anaefaa na wala si mvumilivu, akamwita ‘Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu) afike kwake akafika akiwa na kundi la watu wa Kuufah, akawauliza ‘Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu) wakasema, huyu tunaapa kwa Mwenyezi Mungu kuwa wala hafai wala hajui siasa jambo gani umemtawalisha nalo, ‘Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu) akamuuliza mbele yao kuhusu utawala wake akimjaribu ili ajue kiwango cha uelewa wake katika uongozi akawa hakutoa majibu yaliyomkinaisha ‘Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu) na akamvua madaraka).
(Kitabu cha Taariykh At-Twabariy, juzuu ya 4, uk. 162).


Kauli Ya Aboud Jumbe:(Rais Mstaafu Wa Zanzibar Na ‘‘Makamu Wa Mwenyekiti Wa CCM Mstaafu).
Kwa Uislam basi dini haiwezi kutenganishwa na siasa kwa sababu ni sehemu ya maisha.’’
(Angalia The Partnership uk.131).


Wakristo Wanakiri Kwamba Uislam Ni Njia Kamili Ya Maisha
Katika kitabu “KUWASHIRIKISHA WAISLAMU UPENDO WA MUNGU na Bill Danett UK 21.
“Uislam unaingia katika mambo yote ya maisha”
“Ni muhimu kufahamu kuwa uislam ni njia ya maisha yote. Waislam huamini kuwa ummah wao ndio bora ulio inuliwa kwa ajili ya binadamu (Quraan 3: 110), maongozi ya ummah huo yanathibitika katika uadilifu, usafi, ukarimu, na uhusiano bora katika familia. Uislamu hukusiana na mambo yote ya maisha: dini, maadili, jamii, utamaduni, uchumi, na siasa. Hutawala kila dakika ya maisha yao saa ishirini na nne kila siku tangu kuzaliwa hadi kufa. Mwislamu si mtu binafsi tu, bali mshiriki katika jamii iliyo na uhusiana wa karibu sana na ndani ya jamii hii, ushiriki pia katika familia yenye uhusiano uliyo wa karibu hapa zaidi.
(Kimechapwa 1992 na life challenge Africa s.l.p 50770, city square 00200, Nairobi, Kenya).


Wakristo Nao Pia Wanakiri Kwamba Uislam Haukutenganisha Dini Na Siasa Tangu Zamani

Anasema Fredrick Fredolin Portmann katika kitabu chake: DINI MBALI MBALI NA UTUME WETU.
“Zamani Quraan ilikuwa sheria ya maisha yote si ya dini tu, ila pia ya serikali na siasa’’ uk. 30

Mfumo wa kutenganisha dini na siasa (mamlaka ya nchi) ni wa kikristo, na Waingereza (wakristo) walipoasisi katiba ya nchi hii ndio walituwekea msingi huu, Katika Biblia Yesu amenukuliwa akisema,
“Basi mpeni Kaizari vilivyo vyake na vya Mungu vilivyo vyake (Matayo 22:20) na amesema ufalme wangu sio wa ulimengu huu’’ (Yohana 18:36)


Katika Kitabu Wana wa Ibrahim UK. 156, chasema hivi:
A. Kwa waislamu mungu na kaysar ni mmoja, yaani asili ya uislamu ilitaka kuchanganya dini na utawala, muhammad alianzisha ujamaa wa pekee ukiwa na sheria ambamo kuna siasa na utawala, na dini na sheria mbali mbali kuhusu yatima, urithi, ndoa, uhusiano na wanafiki, na wapagani, usafi na unajisi, vita na jihadi kisasi, namna ya kuwaendea mahaini na watumwa na wanawake.hayo yote yanaitwa “hudud Allaah” yaani sheria za mungu (kuran 2:188) ni kama mipaka ambayo hairuhusiwi kuivuka”.
B. Wakristo waliotaka utawala wa kidini katika karne zilizopita hawakufanya vile kwa agizo la yesu, kwa sababu agizo lake ni hili: ”vya kaesari, mpeni kaesari, na vya mungu mpeni mungu (lk 20: 25) maana yake wapeni watawala heshima na utii wanayostahili katika mambo ya dunia, na mpeni mungu heshima na utii katika mambo ya roho. Yesu hataki kuchanganya ufalme wa dunia na ufalme wa mungu…dini ni tofauti na serikali, kwa vile dini inaweza kuwashauri watawala ili watawale vyema (ef:6:9) lakini hautaki kutawala badala yao… uk. 158.


4. Siasa Ya Ujamaa

Maana ya Ujamaa ni mfumo wa fikra za kisiasa na uchumi ambazo zimejengwa katika kuamini kwamba kila mtu ana haki sawa katika kupata sehemu ya utajiri wa nchi na kwamba serikali ndiyo inayomiliki njia zote kuu za uchumi.
Uislam haujapinga mtu binafsi kujitajirisha maadamu anatoa Zakaah.

قال تعالى: ﴿ لِلرِّجَالِ نَصِيبٌ مِمَّا اكْتَسَبُوا وَلِلنِّسَاءِ نَصِيبٌ مِمَّا اكْتَسَبْنَ ﴾ (النساء:٤).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Wanaume wana fungu katika mali walizochuma na wanawake wana fungu katika mali walizochuma”
(Surat An-Nisaa: 4).

وقال تعالى: ﴿ وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآَتُوا الزَّكَاةَ﴾ (البقرة:٤٣).
Na Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Na simamisheni Swalah na toeni Zakaah.’’
(Surat Al-Baqarah: 43).

وقال تعالى: ﴿ أَهُمْ يَقْسِمُونَ رَحْمَةَ رَبِّكَ نَحْنُ قَسَمْنَا بَيْنَهُمْ مَعِيشَتَهُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَرَفَعْنَا بَعْضَهُمْ فَوْقَ بَعْضٍ دَرَجَاتٍ لِيَتَّخِذَ بَعْضُهُمْ بَعْضًا سُخْرِيًّا وَرَحْمَةُ رَبِّكَ خَيْرٌ مِمَّا يَجْمَعُونَ ﴾ (الزخرف:٣٢).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala)
“Je wao ndio wanaogawa Rehema za Mola wako?! Sisi ndio tuliogawa maisha yao hapa duniani na tukawanyanyua baadhi yao kuwazidi wengine kwa daraja nyinyi ili wawafanye baadhi yao wengine kuwa watumishi wao, na rehema ya Mola wako bora kuliko kile wanachokikusanya”
(Surat Az-Zukhruf: 32).


وقال صلى الله عليه وسلم:(فأعلمهم أن الله فرض عليهم صدقات تأخذ من أغنيائهم وترد على فقرائهم)(رواه البخاري).
Na amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam): ‘‘Na waelimishe kuwa Allaah Amewawajibishia Sadaka (Zakaah) ambayo huchukuliwa kutoka kwa matajiri wao na kurudishwa kwa masikini wao.’’
(Ameipokea Imaam Al-Bukhaariy).

Uislam hauna mipaka ya kujitajirisha maadamu chumo ni la halali, na hakuna sera za kutaifisha mali za watu kwa dhulma.

قال تعالى: ﴿ وَلَا تَأْكُلُوا أَمْوَالَكُمْ بَيْنَكُمْ بِالْبَاطِلِ وَتُدْلُوا بِهَا إِلَى الْحُكَّامِ لِتَأْكُلُوا فَرِيقًا مِنْ أَمْوَالِ النَّاسِ بِالْإِثْمِ وَأَنْتُمْ تَعْلَمُونَ﴾ (البقرة:١٨٨).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Na wala msile mali zenu kati yenu kwa batili na kuzipeleka kwa mahakimu ili mpate kula sehemu ya mali za watu kwa dhambi na nyinyi mnajua”
(Surat Al-Baqarah: 188).

Kwa siasa ya ujamaa watu walidhulumiwa haki zao kwa uonevu kwamba ni mabepari na mabwenyenye, makabaila na wanyonyaji kinyume hata na katiba ya nchi kifungu No.22 (2):
Bila ya kuathiri masharti ya ibara ndogo ya (1): ni marufuku kwa mtu yeyote kunyang’anywa mali yake kwa madhumuni ya kuitaifisha au madhumuni mengineyo bila ya idhini ya sheria ambayo inaweka masharti ya kutoa fidia inayostahili.


5. Mfumo Wa Kukataza Kuanzisha Chama Cha Siasa Chenye Lengo La Kukuza Dini

Katika Uislamu mfumo huu haukubaliki kwa sababu Dini ndio inayotuongoza katika kila kitu amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
قال تعالى:﴿ شَرَعَ لَكُمْ مِنَ الدِّينِ مَا وَصَّى بِهِ نُوحًا وَالَّذِي أَوْحَيْنَا إِلَيْكَ وَمَا وَصَّيْنَا بِهِ إِبْرَاهِيمَ وَمُوسَى وَعِيسَى أَنْ أَقِيمُوا الدِّينَ وَلَا تَتَفَرَّقُوا فِيهِ﴾(الشورى:١٣).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
‘‘Amekuwekeeni shari’ah itokanayo na Dini aliyomuusia Nuuh na ambayo tumekuteremshia wahyi kwako na tuliyomuusia Ibraahiym na Muusa na ‘Iysa kwamba musimamishe Dini wala msifarikiane (kwenye Dini).’’
(Surat Ash-Shuuraa: 13).

وقال تعالى:﴿ قُلْ هَذِهِ سَبِيلِي أَدْعُو إِلَى اللَّهِ عَلَى بَصِيرَةٍ﴾(يوسف:١٠٨).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
‘‘Waambie hii ndio ndio njia yangu nalingania kwa Allaah kwa ujuzi)”
(Surat Yuusuf: 108).
Kutangaza Dini ni wajibu wa kila Muislam akiwapo mwanasiasa, lakini katiba inazuia mwanasiasa kusimamisha dini.


6. Sera Ya Kulazimisha Kila Raia Kufuata Na Kutii Katiba Na Sheria Za Nchi Hata Zikikhalifu Shari’ah Ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) (Kitabu Na Sunnah)

Waislamu wanalazimika kufuata shari’ah za Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) na sio za twaghuut.

قال تعالى:﴿ أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ يَزْعُمُونَ أَنَّهُمْ آَمَنُوا بِمَا أُنْزِلَ إِلَيْكَ وَمَا أُنْزِلَ مِنْ قَبْلِكَ يُرِيدُونَ أَنْ يَتَحَاكَمُوا إِلَى الطَّاغُوتِ وَقَدْ أُمِرُوا أَنْ يَكْفُرُوا بِهِ وَيُرِيدُ الشَّيْطَانُ أَنْ يُضِلَّهُمْ ضَلَالًا بَعِيدًا﴾(النساء:٦٠).
Amesema Allaah: (Subhaanahu wa Ta’ala):
‘‘Hivi hauwaoni wale ambao wanadai kwamba wameamini yale yaliyoteremshwa kwako na yaliyoteremshwa kabla yako (kisha) wanataka wahukumiwe na Twaghuti (asiekuwa Allaah) hali ya kuwa wameamrishwa kumkufuru huyo (Twaghuti) na anataka Shaytwaan kuwapotosha upotoshi wa mbali)”
(Surat An-Nisaa: 60).

Waislam tunaamrishwa kufuata Qur-aan:

وقال تعالى:﴿ وَهَذَا كِتَابٌ أَنْزَلْنَاهُ مُبَارَكٌ فَاتَّبِعُوهُ وَاتَّقُوا لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ ﴾(الأنعام:١٥٥).
Na Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Na hiki Kitabu Tumekiteremsha chenye Baraka kifuateni na mcheni (Allaah) ili mpate kurehemewa”
(Surat Al-An’aam: 155).

وقال تعالى:﴿ ثُمَّ جَعَلْنَاكَ عَلَى شَرِيعَةٍ مِنَ الْأَمْرِ فَاتَّبِعْهَا وَلَا تَتَّبِعْ أَهْوَاءَ الَّذِينَ لَا يَعْلَمُونَ ﴾(الجاثية:١٨).
Na Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Kisha tukakufanya ufuate shari’ah itokanayo na amri (ya Allaah) ifuate shari’ah hiyo wala usifuate matamanio ya wale wasiojua)”
(Surat Al-Jaathiyah: 18).

وقال تعالى:﴿ وَإِنَّ الشَّيَاطِينَ لَيُوحُونَ إِلَى أَوْلِيَائِهِمْ لِيُجَادِلُوكُمْ وَإِنْ أَطَعْتُمُوهُمْ إِنَّكُمْ لَمُشْرِكُونَ﴾(الأنعام:١٢١).
Na Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Na hakika Mashaytwaan huwatia maneno wapendwa wao ili wakujadilini (kwa kupinga) na kama mkiwatii hakika yenu nyinyi mtakuwa ni washirikina”
(Surat Al-An’aam: 121).

وقال صلى الله عليه وسلم: لا طاعة المخلوق في معصية الخالق(رواه البخاري)
Na amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam):
”Hakuna kumtii kiumbe kwenye jambo la kumuasi Muumba”
(Ameipokea Imaam Al-Bukhaariy).
لما بايع المسلمون أبابكر الصديق رضي الله عنه بيعة .... في السقيفة جلس في اليوم التالي للبيعة العامة ثم قام خطيبا في الناس فحمد الله وأثنى عليه بما هو أهله ثم قال:أما بعد ايها الناس فإني قد وليت عليكم ولست بخيركم فإن أحسنت فأعينوني وإن أسأت فقوموني الصدق أمانة والكذب خيانة والضعيف فيكم قوي عندي حتى آخذ علته إن شاء الله وإن القوي فيكم ضعيف حتى آخذ منه الحق إن شاء الله لا يدع القوم الجهاد في سبيل الله إلا جربهم الله بالذل ولا تشيع الفاحشة في قوم إلا عمهم الله بالبلاء اطيعوني ما أطعت الله ورسوله فإن عصيت الله ورسوله فلا طاعة لي عليكم.(السيرة لابن كثير ج\٣ ص ٤٩٢ ط\دار المعرفة)
“Walipomba’ii (kumkubali kuwa kiongozi) waislamu Abu Bakr (Radhiya Allaahu ‘anhu) katika bustani alikaa siku ya pili yake ili aba’iiwe na watu wote kisha akasimama na kuhutubu akasema: ‘‘Baada ya hayo, enyi watu mimi nimetawalishwa kuwa mtawala wenu lakini sio mimi ndio mbora wenu kama nikifanya vizuri nisaidieni na kama nikifanya vibaya nirekebisheni, ukweli ni amana na uongo ni hiyana dhaifu wenu kwangu ndio mwenye nguvu mpaka nimrejeshee haki yake, na mwenye nguvu kwenu ni dhaifu kwangu mpaka nichukue haki yake, In-shaa Allaah., hawatoacha watu jihadi katika njia ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) isipokuwa Mwenyezi Mungu huwapa udhalili na hayataenea maovu kwa watu isipokuwa Allaah Atawanezea mabalaa. Nitiini muda nitakapokuwa namtii Allaah na Mtume Wake na kama nikimuasi Allaah na Mtume Wake msinitii” (Kitabu Ibn Kathiyr Juzuu 3, uk. 492, chapa ya Daar Al Maarifah).

قال تعالى:﴿ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آَمَنُوا أَطِيعُوا اللَّهَ وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ وَأُولِي الْأَمْرِ مِنْكُمْ﴾(النساء:٥٩).
Na amsema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“(Enyi ambao mlioamini mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume na waliotawalia mambo miongoni mwenu”
(Surat An-Nisaa: 59).

عن ابن عمر رضي الله عنهما أن النبي صلى الله عليه وسلم قال:(على المرء المسلم السمع والطاعة فيما أحب وكره إلا أن يؤمر بمعصية فإذا امر بمعصية فلا سمع ولا طاعة)(متفق عليه).
Na amepokea Ibn ‘Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam) amesema: ”Inampasa Muislamu kusikia na kutii kwenye kitu anachokipenda au anachokichukia isipokuwa akiamrishwa Maasi kama akiamrishwa Maasi asisikilize wala kutii” (Wameipokea Al-Bukhaariy na Muslim).



7. Kiongozi Wa Nchi Kupewa Madaraka Ya Kusamehe Au Kupunguza Adhabu

Katika Uislam kiongozi anaweza kusamehe au kupunguza adhabu za taaziyr tu na hana uwezo wa kusamehe huduud na haki za watu.

أسامة بن زيد شفع لدى رسول الله صلى الله عليه وسلم في المرأة المخزومية:(قرشية التي سرقت فقال صلى الله عليه وسلم:ياأسامة أتشفع في حد من حدود الله ثم قام فقال:إنما هلك الذين من قبلكم أنهم كانوا إذا سرق فيهم الشريف تركوه،وإذا سرق الضعيف اقاموا عليه الحد وأيم اتلله لو أن فاطمة بنت محمد سرقت لقطعت يدها.(رواه البخاري).
“Swahaba Usaamah bin Zayd alitaka alimwombea kwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) mwanamke wa koo la Makhzumiy litokanalo na kabila la ma-Quraysh mwanamke ambae aliiba. Mtume akamwambia Usama: ‘‘Ewe Usaamah unafanya maombezi kwenye Had (Adhabu) miongoni mwa Huduud za Allaah, kisha akatoa khutbah Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) akasema: ‘‘Hakika waliangamia waliokuwa kabla yenu ilkuwa akiiba mtukufu miongoni mwao humuacha (bila ya Adhabu) na kama akiiba dhaifu humsimamishia Had (Adhabu) juu yake. Naapa kwa Allaah hata kama Faatwimah bint Muhammad (yaani binti yake) akiiba nitakata mkono wake”
(Ameipokea Al-Bukhaariy).



8. Uhuru Wa Kubalidisha Dini

Katika Uislamu mtu akishakuwa Muislamu basi hana uhuru kubalidilisha dini na akibalidisha basi atatakiwa arudi na akikataa basi anauawa.
قال صلى الله عليه وسلم:(من بدل دينه فاقتلوه)(رواه البخاري).
Amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam):
”(Mwenye kubadili Dini yake (Uislamu) basi muueni)” (Ameipokea Al-Bukhaariy).

قال تعالى:﴿ وَمَنْ يَرْتَدِدْ مِنْكُمْ عَنْ دِينِهِ فَيَمُتْ وَهُوَ كَافِرٌ فَأُولَئِكَ حَبِطَتْ أَعْمَالُهُمْ فِي الدُّنْيَا وَالْآَخِرَةِ وَأُولَئِكَ أَصْحَابُ النَّارِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ﴾(البقرة:٢١٧).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Mwenye kuacha Dini yake miongoni mwenu na akafa hali ya kuwa ni kafiri hao matendo yao yatakuwa yameporomoka duniani na akhera na hao ni watu wa motoni watakaa humo milele”
(Surat Al-Baqarah: 217).

ويقول رسول الله صلى الله عليه وسلم:(لا يحل دم امرئ مسلم يشهد أن لاإله إلا الله وأني رسول الله إلا بإحدى ثلاث:الثيب الزاني،والنفس بالنفس والتارك لدينه المفارق للجماعة(رواه البخاري).
Na anasema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam):
”Si halali (haramu) kuimwaga damu ya Muislamu yeyote mwenye kushuhudia kwamba hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah na mimi ni Mtume wa Allaah isipokuwa kwa kufanya moja ya mambo matatu: mzinifu alieoa au kuolewa, aliyeua, aliyeiacha Dini yake mwenye kuacha umoja”
(Ameipokea Al-Bukhaariy).


Shubha: (Hoja ya wapinzani)
Msimano huu wa Uislam ni kinyume na Tangazo la ulimwengu la Haki za Binaadam la mwaka 1945 kifungu 18(b) kwa mtu ana uhuru wa kubalidisha dini anayotaka

Jawabu:
La kushangaza katika nchi nyingi za kisekula mtu akifanya kosa la uhaini (treason) anauliwa kwa sababu tu amekwenda kinyume na nidhamu ya Dola kwa lengo la kugeuza nidhamu ya utawala uliopo, mbona Uislamu unalaumiwa kwa jambo ambalo likifanywa na wengine hawalaumiwi?



9. Sera Ya Kuupapatikia Uongozi Na Kuugombania

Katika Uislam ni Haramu mtu kuomba au kupapatikia uongozi.

عن أبي موسى الأشعري رضي الله عنه قال:(دخلت على النبي صلى الله عليه وسلم أنا ورجلان من الأشعريين فقال أحدهما يارسول الله أمرنا على بعض ما ولاك الله وقال الآخر مثل ذلك فقال:إنا لا نولي على هذا العمل أحدا سأله ولا أحد حرص عليه قال صلى الله عليه وسلم لعبد الرحمن بن صخرة :ياعبدالرحمن لا تسأل الإمارة فإنك إن أعطيتها عن مسألة وكلت إليها وإن أعطيتها من غير مسألة أعنت عليها(رواه مسلم).
Imepokewa kutoka kwa Abuu Muusa Al-Ash’ariy (Radhiya Allaahu ‘anhu) Amesema: ”Niliingia kwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam) mimi na watu wengine wawili watokanao na Al-Ash’ariy (koo/kabila) mmoja wao akasema ewe mjumbe wa Mwenyezi Mungu nipe uongozi kwenye baadhi ya vile alivyokutawalisha Allaah, na yule mwingine akasema hivyo hivyo. Akasema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam) sisi hatumpi kazi hii ya uongozi mtu yeyote yule aliyeiomba au mtu aliyepupia, akasema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam) kwa Abdur-Rahmaan Ibn Swakhrah (Radhiya Allaahu ‘anhu): Ewe Abdur-Rahmaan usiuombe uongozi kwani wewe ukipewa huo uongozi kwa kuuomba utaachiwa bila kusaidiwa na kama ukipewa uongozi bila ya kuuomba utasaidiwa”
(Ameipokea Muslim).

عن أبي هريرة رضي الله عنه:أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال:إنكم ستحرصون على الإمارة وستكون ندامة يوم القيامة(رواه البخاري).
Amepokea Abuu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam) amesema:
”Hakika nyinyi mtapapia uongozi kisha itakuwa ni majuto kweni siku ya Qiyaamah”
(Ameipokea Al-Bukhaariy).



10. Mfumo Wa Vyama Vingi Vya Kisiasa

Katika Uislam vyama ni viwili (2) tu chama cha Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) na chama cha Shaytwaan.
Si ruhusa katika Uislam kuunda makundi ambayo hujiita vyama vya upinzani kazi yao ni kupinga serikali iliyo madarakani haijawahi kutokea tangu zama za Makhalifa hadi Khalifa wa Mwisho hakujawa na mfumo wa vyama vingi.
Sera ya vyama vingi umeasisiwa Firauni na hatimae imeletwa na Makafiri hapa nchini.

قال تعالى:﴿ إِنَّ فِرْعَوْنَ عَلَا فِي الْأَرْضِ وَجَعَلَ أَهْلَهَا شِيَعًا يَسْتَضْعِفُ طَائِفَةً مِنْهُمْ﴾(القصص:٤).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Hakika Firauni alijikweza katika hii Ardhi na kuwagawa watu wake makundi tofauti na akawadhoofisha baadhi yao”
(Surat Al-Qaswasw: 4).

Katika kitabu: ELIMU YA DEMOKRASIA SHIRIKISHI (Kitabu cha 4 kimotolewa na C.P.T. DSM UK.7:
“Wanasayansi wa mambo ya siasa wanaelekea kukubali kwamba demokrasia ya vyama vingi imeanzishwa toka nje kwa kutokana na shinikizo la masharti ya kupata misaada ya fedha.’’


Uislamu Unatutaka Waislam Tuwe Kitu Kimoja

قال تعالى:﴿ وَاعْتَصِمُوا بِحَبْلِ اللَّهِ جَمِيعًا وَلَا تَفَرَّقُوا﴾(آل عنران:١٠٣).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Shikamaneni na kamba (Dini) ya Mwenyezi Mungu nyote wala msitofautiane”
(Al-‘Imraan 103).

وقال تعالى:﴿ إِنَّ الَّذِينَ فَرَّقُوا دِينَهُمْ وَكَانُوا شِيَعًا لَسْتَ مِنْهُمْ فِي شَيْءٍ﴾(الأنعام:١٥٩).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Hakika wale ambao wameacha Dini zao na kuwa makundi makundi wewe hauhusiki nao kwa lolote.”
(Surat Al-An’aam: 159).


11. Kiongozi Wa Nchi (Rais) Kuwa Juu Ya Sheria

Katika Uislam mtawala na mtawaliwa wote wako sawa katika sheria.
قال صلى الله عليه وسلم:(لو أن فاطمة بنت محمد سرقت لقطعت يدها)(رواه البخاري).
Amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam): ”Hata kama Faatwimah mtoto wa Muhammad akiiba nitakata mkono wake”
(Imepokewa na Al-Bukhaariy).


Kisa cha Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam) alipowaaga Waislam
Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam) wakati wa maradhi yake aliyokufa nayo alitoka nje kwa kutolewa na Al-Fadhli bin ‘Abbaas (Radhiya Allaahu ‘anhu) na ‘Alliy bin Abi Twaalib (Radhiya Allaahu ‘anhu) na kuwekwa juu ya mimbari kisha akasema:
(أيها الناس من كنت جلدت له ظهرا فهذا ظهري فليستقد منه ومن كنت شتمت له عرضا فهذا عرضي فليستقد منه ومن أخذت له مالا فهذا مالي فليأخذ ماله ولا يخشى الشحناء من قبلي فإنها ليست من شأني ألا وإن أحبكم إلي من أخذ مني حقا إن كان له أو حللت فلقيت ربي وأنا طيب النفس ثم نزل فصلى الظهر ثم رجع إلى المنبر فعاد لمقالته الأولى(الكامل في التاريخ ج٢ ص ١٣٢ لابن الآثير).
“Enyi watu yoyote yule ambaye nimemchapa mgongo wake basi huu ni mgongo wangu na aje kulipiza kisasi, na kwa yule ambaye nimemvunjia heshima yake basi hii ni heshima yangu na aje kulipiza kisasi na yule niliyemchukulia mali yake basi hii ni mali yangu na aje kuchukua haki yake, na wala usiogopwe uadui toka kwangu kwani hilo sio katika shani yangu, na mjue kuwa kipenzi zaidi kwangu katika nyinyi ni yule aliechukua haki yake toka kwangu na akanisamehe na nikakutana na Mola wangu hali ya kwamba nafsi yangu imetakasika, kisha akashuka na kuswali Adhuhuri kisha akarejea kutamka maneno yake ya mwanzo.
(Angalia Kitabu Al-Kaamil Fiy Taariykh Juzuu 2, uk. 132 cha Ibn Athiyr).


Kisa Cha Khalifa ‘Alliy Alipomushtaki Yahudi Mbele Ya Qaadhi Shurayh

Ambapo Khalifa alipoteza ngao yake ya vita, kisha akaiona kwa Myahudi hakuichukua kutoka kwake bali alimshitaki kwa Qaadhi mkuu Shurayh, akakosa Khalifa ushahidi, akahukumu Qaadhi Shurayh kuwa ile ngao ni ya Yahudi, na hivyo Yahudi kuwa ni mshindi katika kesi hii.

عَنْ أَبِى فِرَاسٍ قَالَ: خَطَبَنَا عُمَرُ بْنُ الْخَطَّابِ رَضِىَ اللَّهُ عَنْهُ فَقَالَ فِى خُطْبَتِهِ: أَلاَ وَإِنِّى لَمْ أَبْعَثْ إِلَيْكُمْ عُمَّالِى لِيَضْرِبُوا أَبْشَارَكُمْ وَلاَ لِيَأْخُذُوا أَمْوَالَكُمْ وَلَكِنْ بَعَثْتُهُمْ لِيُعَلِّمُوكُمْ دِينَكُمْ وَسُنَنَكُمْ فَمَنْ فُعِلَ بِهِ غَيْرُ ذَلِكَ فَلْيَرْفَعْهُ إِلَىَّ فَأُقِصَّهُ مِنْهُ. من كتاب السنن الكبرى للبيهقي.
Imepokewa Na Abuu Firaasi Amesema:
”Alihutubu ‘Umar Ibn Al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ‘anhu) akasema katika hotuba yake, ‘‘Eleweni kuwa mimi sijawatuma kwenu viongozi wangu ili wawapige na kuchukua mali zenu lakini nimewatuma kwenu ili wawafundisheni Dini yenu na Sunnah zenu atakaefanyiwa kinyume na hivyo basi ashitaki kwangu na nitamlipizia kisasi kwa huyo kiongozi”.
(As-Sunanu Al-Kubraa ya Imaam Al Bayhaqiy).

عَنْ أَبِى سَعِيدٍ الْخُدْرِىِّ قَالَ: بَيْنَا رَسُولُ اللَّهِ –صلى الله عليه وسلم يَقْسِمُ شَيْئًا أَقْبَلَ رَجُلٌ فَأَكَبَّ عَلَيْهِ فَطَعَنَهُ رَسُولُ اللَّهِ –صلى الله عليه وسلم بِعُرْجُونٍ كَانَ مَعَهُ فَجُرِحَ الرَّجُلُ فَقَالَ لَهُ رَسُولُ اللَّهِ –صلى الله عليه وسلم:« تَعَالَ فَاسْتَقِدْ ». فَقَالَ: بَلْ عَفَوْتُ يَا رَسُولَ اللَّه(من كتاب السنن الكبرى للبيهقي)

Na imepokewa na Abu Sa’id Al-Khudriy amesema: ”Wakati Mtume anagawa kitu fulani ghafla akatokea mtu na kumwangukia, akmchoma Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam) yule mtu na mti aliokuwa ameushika na kumjeruhi, Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam) akamwambia yule mtu njoo ulipize kisasi, akasema: '‘Bali nimesamehe ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu).
(As-Sunanu Al-Kubraa ya Imaam Al Bayhaqiy).


12. Sera Ya Kukataza Matumizi Ya Nguvu (Jihadi) Katika Kufikia Malengo Ya Kisiasa

Uislam haujakataza moja kwa moja kutumia nguvu katika kudai haki hasa kama mtawala anafanya dhulma za wazi na Waislamu wakiwa wamejianda kwa nguvu za silaha.

قال تعالى:﴿ وَأَعِدُّوا لَهُمْ مَا اسْتَطَعْتُمْ مِنْ قُوَّةٍ وَمِنْ رِبَاطِ الْخَيْلِ تُرْهِبُونَ بِهِ عَدُوَّ اللَّهِ وَعَدُوَّكُمْ﴾(الأنفال:٦٠).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Waandalieni hao (makafiri) kila mnachokiweza katika nguvu na na ngome ya farasi ili muwatishe maadui wa Allaah na maadui wenu”
(Surat Al-Anfaal: 60).

وقال تعالى:﴿ إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ الَّذِينَ آَمَنُوا بِاللَّهِ وَرَسُولِهِ ثُمَّ لَمْ يَرْتَابُوا وَجَاهَدُوا بِأَمْوَالِهِمْ وَأَنْفُسِهِمْ فِي سَبِيلِ اللَّهِ أُولَئِكَ هُمُ الصَّادِقُونَ ﴾(الحجرات:١٥).
Na Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Hakika Waumini wa kweli ni wale ambao wamemuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake kisha hawakuingiwa na mashaka na wakapigana kwa mali zao na nafsi zao katika njia ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) hao ndio waumini wa kweli kabisa”
(Surat Al-Hujuraat: 15).

وقال تعالى:﴿ أَمْ حَسِبْتُمْ أَنْ تَدْخُلُوا الْجَنَّةَ وَلَمَّا يَعْلَمِ اللَّهُ الَّذِينَ جَاهَدُوا مِنْكُمْ وَيَعْلَمَ الصَّابِرِينَ ﴾(آل عمران:١٤٢).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Hivi mnadhani kuwa mtaingia peponi kabla ya (kujaribiwa) na Allaah na kujua ni wapi kati yenu wenye kuipigania Dini ya Allaah na ni wapi wenye Subira”
(Surat Al-‘Imraan: 142).

وقال تعالى:﴿ وَقَاتِلُوهُمْ حَتَّى لَا تَكُونَ فِتْنَةٌ وَيَكُونَ الدِّينُ لِلَّهِ﴾(البقرة:١٩٣).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Na wapigeni vita hao (makafiri) mpaka kusiwe na fitna na iwe Dini ni ya Allaah (inayofuatwa)”
(Surat Al-Baqarah: 193).

Ulimwengu umekiri matumizi ya nguvu katika nchi zifuatazo baada ya raia kudhulumiwa haki zao :
-Zanzibar katika mapinduzi ya mwaka 1964
-Msumbiji na Frelimo
-Kenya na Mau Mau
-Biafra Nigeria na Rais Nyerere alishabikia mtengano kwa sababu wakristo walikuwa wakidhulumiwa na Waislamu na aliandika kitabu 1966 (rejea gazeti la Majira la tarehe 16/11/2011 Uk.3) akidai kwamba umoja wa Kitaifa hauna maana endapo baadhi ya raia wanadhulumiwa.


13. Sera Ya Kukanusha Itikadi Ya Al-Walaa Wal-Baraa

Katika Uislam kutobaguana kwa msingi wa kidini ni kinyume cha Itikadi muhimu ya Al-Walaa wal-Baraa (kupendana na kuchukiana kwa ajili ya Allaah).
Udugu unaokubalika katika Uislam ni wa Imani tu.

﴿إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ﴾(الحجرات:١٠).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Hakika waumini (tu) ndio ndugu”
(Al-Hujuraat:10).

Kafiri sio ndugu wala rafiki wa waumini.
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
﴿قَدْ كَانَتْ لَكُمْ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ فِي إِبْرَاهِيمَ وَالَّذِينَ مَعَهُ إِذْ قَالُوا لِقَوْمِهِمْ إِنَّا بُرَآَءُ مِنْكُمْ وَمِمَّا تَعْبُدُونَ مِنْ دُونِ اللَّهِ كَفَرْنَا بِكُمْ وَبَدَا بَيْنَنَا وَبَيْنَكُمُ الْعَدَاوَةُ وَالْبَغْضَاءُ أَبَدًا حَتَّى تُؤْمِنُوا بِاللَّهِ وَحْدَهُ﴾(الممتحنة:٤).
“Hakika kuna mfano mzuri kwenu kwa Ibraahiym na walio pamoja nae waliopowaambia watu wao, sisi tuko mbali na nyinyi na yale mnayoyaabudu badala ya Allaah tumewakanusha nyinyi na umedhihiri uadui na bughdha baina yetu sisi na baina yenu milele mpaka mumuamini Allaah Peke yake.’’
(Al-Mumtahinah: 4)

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آَمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا عَدُوِّي وَعَدُوَّكُمْ أَوْلِيَاءَ تُلْقُونَ إِلَيْهِمْ بِالْمَوَدَّةِ وَقَدْ كَفَرُوا بِمَا جَاءَكُمْ مِنَ الْحَقِّ﴾(الممتحنة:١)
Na amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Enyi Mlioamini msiwafanye adui yangu na adui wenu kuwa ni marafiki (wasaidizi) mna waangushia mapenzi na kwa hakika wamekufuru yale yaliowajieni katika haki”
(Al-Mumtahinah: 1)

Ama kubaguana kwa misingi ya Utaifa, Ukabila, Urangi, Uzawa, Uzalendo na msingi wa Kilugha ni jambo lililokatazwa katika Uislam.

Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
﴿يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّا خَلَقْنَاكُمْ مِنْ ذَكَرٍ وَأُنْثَى وَجَعَلْنَاكُمْ شُعُوبًا وَقَبَائِلَ لِتَعَارَفُوا إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِنْدَ اللَّهِ أَتْقَاكُمْ﴾(الحجرات:١٣)
“Enyi watu hakika sisi tumewaumbeni kutokana na mwanamme mmoja na mwanamke mmoja na tukawajaalia kuwa mataifa mbali mbali na makabila mbali mbali ili mjuane, hakika mbora wenu mbele ya Allaah ni Mcha Mungu wenu zaidi.”
(Al-Hujuraat: 13).

Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) alikemea sana ugomvi baina ya Muhajirina (waliohama toka Makkah) na Answaar (wazawa wa Madiynah) kwa misingi ya Uzawa na Akasema:
“Enyi Waislam (mnagombana) kwa wito wa msingi wa Kijahiliya (Kikafiri) na mimi niko pamoja nanyi baada ya Allaah kuwaongoza katika Uislam? Uacheni kwani huo ni uvundo”

SURA YA SITA

Tafsiri Sahihi Ya Baadhi Ya Maneno Na Vifungu Vya Katiba Ya Jamhuri


1. Neno Ibada: Kwa Mtazamo Wa Uislam Ni Pana Sana

Wanachuoni wetu wanakubaliana kwamba ibada ni:
"كل ما يحب الله ويرضاه من الأقوال والأعمال الظاهرة والباطنة”
“Ni kila anachokipenda Mwenyezi Mungu na kukiridhia katika maneno na matendo ya dhahiri na ya siri (moyoni)”.

Malengo ya Kuumbwa kwetu:
قال تعالى:﴿ وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنْسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ﴾(الذريات:٥٦).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Sikuumba majini na watu isipokuwa kwa ajili ya kuniabudu Mimi tu”
(Adh-Dhaariyaat: 56).

Kumuabudu Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) hakuna maana ya kuswali, kufunga, kuhiji tu. Bali ndoa, kazi, biashara kuhukumiana kwa shari’ah ni ibada.

قال تعالى:﴿ قُلْ إِنَّ صَلَاتِي وَنُسُكِي وَمَحْيَايَ وَمَمَاتِي لِلَّهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ﴾(الأنعام:١٦٢).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Hakika Swalah yangu na Ibada yangu (kuchinja) na uhai wangu na kifo changu ni kwa ajili ya Allaah Mola wa viumbe wote)”
(Surat Al-An’aam: 162).


Kuhukumu kwa haki ni Ibada.

قال تعالى:﴿ إِنِ الْحُكْمُ إِلَّا لِلَّهِ أَمَرَ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا إِيَّاهُ﴾(يوسف:٤٠).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Hukumu ni miliki ya Allaah Ameamrisha musiabudu (chochote) isipokuwa Yeye tu)”
(Surat Yuusuf: 40).

قال شمس الأئمة السرخسى:إعلم أن القضاء بالحق من أقوى الفرائض بعد الإيمان بالله تعالى وهو من أشرف العبادات(المبسوط:١٦٥ ص٥٩،٦٠).
Amesema Shamsu Al-Aimmah As-Sarkhasi:
“Elewa kwamba kuhukumu kwa haki ni miongoni mwa faradhi kubwa baada ya kumwamini Mwenyezi Mungu na hiyo ndio Ibada tukufu”
(Al-Mabsuutw, uk. 59-60).



2. Neno Halali Ni Hukmu Ya Kishari’ah Ni Kila Aliloliridhia Mola Kufanywa Kwa Mujibu Wa Shari’ah

Kwa mujibu wa katiba ukiuza pombe maadam unalipa leseni, kodi na pombe si ya magendo basi kazi hii ni Halali.
Kufanya muamala wa riba ni halali.
Kamari ni halali.

قال تعالى:﴿ إِنَّمَا الْخَمْرُ وَالْمَيْسِرُ وَالْأَنْصَابُ وَالْأَزْلَامُ رِجْسٌ مِنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ فَاجْتَنِبُوهُ﴾(المائدة:٩٠).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Hakika pombe na kamari na mizimu ni uchafu utokanao na matendo ya Shaytwaan jiepusheni nayo”
(Surat Al-Maaidah: 90).

وقال تعالى:﴿ وَأَحَلَّ اللَّهُ الْبَيْعَ وَحَرَّمَ الرِّبَا ﴾(البقرة:٢٧٥).
Na Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Na Amehalalisha Mwenyezi Mungu biashara na ameharamisha riba”
(Surat Al-Baqarah: 275).


3. Neno Haki Ya Kuishi

Mtu akiua hauawi kwa sababu eti ana haki ya kuishi.

Katika kesi ya Attorney (Mwendesha mashtaka wa serikali) V/s Mbushumi (Kesi ya jinai Na.14, Dodoma 1991.) Katika kesi hii mtuhumiwa Mbushumi Mnywaga alikuwa akikabiliwa na kesi ya mauaji ambapo kwa mujibu wa sheria, adhabu yake ni kunyongwa hadi kufa.
Mshtakiwa (mtuhumiwa) katika kesi hii alidai mahakamani haki ya msingi ya kuishi kwa mujibu wa katiba.
Mahakama ilkubaliana nae na hivyo kumhukumu mshitakiwa kwenda jela maisha badala ya kunyongwa hadi kufa.
(Angalia kitabu, Haki na wajibu wa raia uk.23 kilichotolewa na C.P.T (Christian Prof.of Tanzania).

Katika Uislamu mtu anaeua kwa dhulma nae anauliwa kutekeleza kisasi.

قال تعالى:﴿ وَلَكُمْ فِي الْقِصَاصِ حَيَاةٌ يَا أُولِي الْأَلْبَابِ﴾(البقرة:١٧٩).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Na mna (nyinyi) kwenye kisasi uhai enyi wenye akili”
(Surat Al-Baqarah: 179).


4. Haki Ya Usawa Kwa Wote

Katika Uislamu binaadam wote ni sawa katika asili, Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
﴿يَا أَيُّهَا النَّاسُ إِنَّا خَلَقْنَاكُمْ مِنْ ذَكَرٍ وَأُنْثَى وَجَعَلْنَاكُمْ شُعُوبًا وَقَبَائِلَ لِتَعَارَفُوا إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِنْدَ اللَّهِ أَتْقَاكُمْ﴾(الحجرات:١٣)
”Enyi wtu hakika Sisi Tumewaumbeni kutokana na mwanamme mmoja (Aadam) na mwanamke mmoja (Hawwaa) na Tukawajaalia kuwa mataifa mbali mbali na makabila ili mpate kujuana, hakika mbora wenu mbele ya Allaah ni Mcha Mungu zaidi kwenu”
(Surat Al-Hujuraat: 13).

Lakini hii haina maana kwamba mwanamme na mwanamke wamepewa haki na majukumu sawa kwa kila kitu.

Katika tangazo la haki za binaadam:
Kifungu 16(1) la mwaka 1948:
“Mwanamme na mwanamke pindipo wakifikia umri wa baleghe watakuwa na haki ya kuoana na kuasisi familia bila kikwazo kwa sababu ya nasaba, utaifa au dini, kwani wao wote wana haki sawa katika ndoa na wakati wa kusimamisha maisha ya ndoa na wakati wa mtengano’’ (uk.74).

(أنظر كتاب حقوق الإنسان في الإسلام للدكتور سليمان بن عبدالرحمن الحقيل(ط الثانية ١٤١٥ﻫ١٩٩٤ﻡ)
Tazama kitabu cha HAKI ZA BINADAMU KATIKA UISLAMU cha Dr. Suleiman Ibn Abdulrahmani Al Huqail chapa ya pili 1415H, 1994.

Tanzania ilitia saini mkataba wa kimataifa wa haki za binaadam 1966 na ukatiwa katika katiba mwaka 1966 ibara ya 9(f) nayo inasema hivi:
“Kwamba heshima ya binaadam inahifadhiwa na kudumishwa kwa kufuata kanuni za tangazo la dunia kuhusu haki za binaadam”.

قال تعالى:﴿ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آَمَنُوا إِذَا جَاءَكُمُ الْمُؤْمِنَاتُ مُهَاجِرَاتٍ فَامْتَحِنُوهُنَّ اللَّهُ أَعْلَمُ بِإِيمَانِهِنَّ فَإِنْ عَلِمْتُمُوهُنَّ مُؤْمِنَاتٍ فَلَا تَرْجِعُوهُنَّ إِلَى الْكُفَّارِ لَا هُنَّ حِلٌّ لَهُمْ وَلَا هُمْ يَحِلُّونَ لَهُنَّ وَآَتُوهُمْ مَا أَنْفَقُوا وَلَا جُنَاحَ عَلَيْكُمْ أَنْ تَنْكِحُوهُنَّ إِذَا آَتَيْتُمُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ وَلَا تُمْسِكُوا بِعِصَمِ الْكَوَافِرِ﴾(الممتحنة:١٠).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Enyi ambao mulioamini watakapowajieni wanawake Waumini wenye kuhama basi wapeni mtihani Mwenyezi Mungu ni Mjuzi zaidi kuhusu kuamini kwao, kama mkijua kwamba wao ni Waumini basi musiwarejeshe kwa makafiri, hao (wanawake) sio halali kwao wala wao sio halali kwao (kwa vile ni makafiri, na wapeni walichotoa (mahari), na wala si vibaya kwenu kuwaoa wao kama mtawapa mahari zao wala musiwaweke wanawake makafiri katika kifungo cha ndoa zenu”
(Al-Mumtahinah: 10).

Kifungu hiki cha katiba kimempa mwanamke usawa wa mia kwa mia na mwanamme, katika Mirathi na Uongozi.

قال تعالى:﴿ فَلِلذَّكَرِ مِثْلُ حَظِّ الْأُنْثَيَيْنِ﴾(النساء:١٧٢).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Basi mwanamme ana mara mbili ya fungu la mwanamke”. (Surat An-Nisaa: 172).

وقال تعالى:﴿ الرِّجَالُ قَوَّامُونَ عَلَى النِّسَاءِ بِمَا فَضَّلَ اللَّهُ بَعْضَهُمْ عَلَى بَعْضٍ﴾(النساء:٣٤).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Wanaume ni wasimamizi (viongozi) wa wanawake ni katika yale ambayo Mwenyezi Mungu Amewaboresha baadhi yenu kwa baadhi.”
(Surat An-Nisaa: 34).

Waislam hawawezi kuwa sawa na watu waovu:

وقال تعالى:﴿ أَفَنَجْعَلُ الْمُسْلِمِينَ كَالْمُجْرِمِينَ﴾(القلم:٣٥).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Hivi tunawafanya Waislamu ni kama waovu!”
(Surat Al-Qalam: 35).

وقال صلى الله عليه وسلم:(لن يفلح قوم ولو أمرهم امرأة)رواه البخاري.
Amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam): “Hawatofaulu kamwe watu waliomfanya mwanamke kutawalia jambo lao”.
(Ameipokea Imaam Al-Bukhaariy).

Katika tangazo la Haki na Usawa la umoja wa mataifa kafiri anaweza kuwa sawa na muislam, hivyo kafiri anaweza kuoa binti wa Kiislam, katika Uislam jambo hilo halikubaliwi.

قال تعالى:﴿ وَلَا تُنْكِحُوا الْمُشْرِكِينَ حَتَّى يُؤْمِنُوا ﴾(البقرة:٢٢١).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Wala musiwaoze washirikina mpaka waamini”. (Surat al Baqarah:221).

وقال تعالى:﴿ وَلَا تُمْسِكُوا بِعِصَمِ الْكَوَافِرِ﴾(الممتحنة:١٠).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Na wala msiwaweke wanawake wa kikafiri katika kifungo cha ndoa zenu”
(Surat Al-Mumtahinah: 10).


5. Haki Ya Kumiliki

Pamoja na kwamba Uislamu unampa mtu haki ya kumiliki na kutasarafu na mali aliyoichuma,
قال تعالى:﴿ لِلرِّجَالِ نَصِيبٌ مِمَّا اكْتَسَبُوا وَلِلنِّسَاءِ نَصِيبٌ مِمَّا اكْتَسَبْنَ﴾(النساء:٣٢).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Wana wanaume fungu katika vile walivyovichuma na wanawake wana fungu katika vile walivyochuma”
(Surat An-Nisaa: 32).

Lakini, mtu hawezi kumuandikia mrithi wasia na huyo ambaye ameandikiwa wasia haruhusiwi kupewa zawadi ya 1/3 ya mali ya mtu.
قال صلى الله عليه وسلم:(إن الله قد أعطى كل ذي حق حقه فلا وصية للوارث)(رواه أبي داود وابن ماجه).
Amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam): ”Hakika Allaah Amempa kila mwenye haki haki yake, hakuna usia kwa mrithi)”
(Wameipokea Abu Daawuud na Ibn Maajah).

وقال صلى الله عليه وسلم:(الثلث،والثلث كثير(رواه البخاري ومسلم).
Amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam) juu ya kiwango anachostahiki kuandikiwa wasia :
“Theluthi, na theluti pia ni nyingi”
)Wameipokea Imaam Al-Bukhaariy na Muslim).

Sheria za nchi ni kinyume cha hayo kwa madai ya kutetea haki za kikatiba.

Katika kesi ya rufaa Na.5/1997 iliyosikilizwa na mahakama ya rufaa Dsm, kati ya Anwar Z. Mohamed vs Saidi Selemani Masuka, katika hukumu yake June 10, 1997, Jaji Ramadhani alihoji hukumu ya Jaji Msumi ya sept, 5, 1996, aliyetengua wasia unaodaiwa kuachwa na Rukia Ahmed kwamba mume wake Anwar Z. Mohamed arithi mali yake yote.

Katika hukumu yake Jaji Msumi wa mahakama kuu wakati huo alitoa hoja kwmba kwa mujibu wa shari’ah za Kiislam hakuna wasia kwa mrithi na hakuna wasia zaidi ya 1/3 ya mali.

Uamuzi huo wa Jaji Msumi ulipingwa na Jaji Korosso (wakili katika kesi hii) akiitaka mahakama ipuuze na itupilie kwa mbali shari’ah hiyo ya Kiislam kwa madai kwamba inavunja haki ya kikatiba kifungu cha 24 kinachompa mtu haki ya kumiliki na kutumia atakavyo. Hata hivyo Jaji Msumi alisisitiza kwamba Shari’ah na mirathi za Kiislam ni sehemu katika Qur-aan na ni lazima Waislam warithiane kwa Shari’ah hii. Na akaonya kuichezea Shari’ah hiyo ni sawa na kuichezea Qur-aan, jambo ambalo alisema Jaji Msumi hadhani kwamba yupo mtu mwenye kutakia mema nchi hii anaweza kulikaribia.

Jaji Ramadhani kwa upande wake alidai kwamba Jaji Msumi amejichanganya mwenyewe katika hukumu yake kwamba amezingatia “Udini” na uzalendo badala ya sheria. Na alisisitiza kanuni ya kutotambua sheria au kanuni zinazokiuka haki za kikatiba.
Waliotengua hukumu hiyo ni waheshimiwa majaji wa mahakama ya rufaa:
L. M. Makanja, D. Z. Lubavu na B. A. Samatta.

Katika kesi hiyo ya Anwar dhidi ya Saidi aliyekuwa mume wa marehemu Rukia Ahmed mwanamke aliyeolewa na Bw.Saidi. Marehemu aliandika wasia wa mali yake yote kwa mumewe Bw.Saidi akimwacha mwanawe wa kuzaa ndugu Anwar bila ya urithi wowote. Ndugu Anwar alikuwa mtoto wa marehemu lakini kwa mume mwingine. Mtoto wa marehemu alipinga kutambuliwa kwa wasia huo kwani ni kinyume cha Shari’ah za Kiislam na akakoseshwa kurithi.
(Angalia Sheria za Kiislam ya Mirathi na wasia) cha Mahmud A.Sameya uk.91 na 92).


6. Kufuta Adhabu Ya Viboko Ni Kinyume Cha Shari’ah Ya Kiislam

Kifungu 13(6) (e) Kinasema:
Ni marufuku kwa mtu kuteswa kuadhibiwa kinyama au kupewa adhabu zinazomtesa au kumdhalilisha.

Uislam unaruhusu adhabu ya viboko.

قال تعالى:﴿ الزَّانِيَةُ وَالزَّانِي فَاجْلِدُوا كُلَّ وَاحِدٍ مِنْهُمَا مِئَةَ جَلْدَةٍ﴾(النور:٢).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Mzinifu mwanamke na mzinifu mwanaume wapigeni kila mmoja mijeledi mia moja”
(Surat An-Nuur: 2).

وقال تعالى:﴿ وَالَّذِينَ يَرْمُونَ الْمُحْصَنَاتِ ثُمَّ لَمْ يَأْتُوا بِأَرْبَعَةِ شُهَدَاءَ فَاجْلِدُوهُمْ ثَمَانِينَ جَلْدَةً﴾(النور:٤).
Amesema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
”Na wale ambao wanawasingizia machafu wanawake wenye kujihifadhi na (machafu) kisha hawakuleta mashahidi wanne wapigeni mijeledi thamanini”
(Surat An-Nuur: 4).

وقال صلى الله عليه وسلم:(مروا أولادكم الصلاة وهم أبناء سبع واضربوهم عليها إذا بلغوا عشرة)(رواه أبوداود).
Amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa wa sallam):
”Waamrisheni watoto wenu Swalah wakiwa na umri wa miaka saba na wapigeni kwa kuacha Swalah watakapofika umri wa miaka kumi”
(Imepokewa na Abu Daawuud).



HITIMISHO

Wakati tukiwa katika hatua za mwisho za uandishi wa kitabu hiki, wananchi wote tumeshtukiziwa na Mswaada wa Sheria ya mwaka 2011 ambayo umekusudia kuweka masharti ya uanzishaji wa Tume, pamoja na sekretarieti kwa madhumuni ya kuendesha na kusimamia mchakato wa mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Cha kushangaza serikali ilitoa hati ya dharura kwa maana ya kwamba wananchi wachangie maoni juu ya Mswaada huu haraka haraka ili upitishwe na bunge kwa njia ya haraka. Muda uliotolewa ni mfupi mno na vituo vya kutoa maoni, vilipangwa kuwa ni vitatu tu Dar es Salaam, Dodoma na Zanzibar.
Wananchi wengi hawakuridhishwa na mchakato huu, jambo ambalo limepelekea zoezi hili kuakhirishwa ili wananchi wapewe muda zaidi wa kutoa maoni.

Baada ya kufaulu kupata nakala ya Mswaada huu tumegundua Mswaada huu una mapungufu mengi lakini makubwa katika hayo ni lile la kuwafunga wananchi wasiyaguse yale ambayo kwa mtazamo wa waliotunga Mswaada huu ni tunu na maadili matakatifu ya kitaifa hivyo yasipingwe katika hayo ni yale yaliyokuja katika kipengele cha 9 (2) :
(a) Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
(b) Msingi /Asili ya Usekula (kutenganisha siasa na dini) ya Jamhuri ya Muungano.

Masharti haya hayakubaliki kwa sababu yanawanyima raia ambao ndio watunzi halisi wa katiba, Uhuru wa Maoni ambao wamepewa na kipengele cha 18 (1) na 19 (1) cha Katiba ya nchi hii.

Upande wetu Waislamu wazo la kuifanya nchi hii idumu kuwa ni ya kisekula inayotenganisha Dini na Utawala ni wazo lisilokubalika hasa ukizingatia kwamba wazo lenyewe asili yake ni Dini ya Kikristo kama tulivyoona katika kitabu hiki. Wazanzibari kwa mfano ambao wana nchi yao yenye wakazi asilimia 99 Waislam wana haki ya kutangaza kwamba nchi yao ni ya Kiislamu yenye kufuata Shari’ah za Kiislam, wenyewe wana haki ya kufanya maamuzi haya.

Kitabu hiki tunataraji kitakua ni msaada mkubwa wa Rejea kwa kila anaetaka kuchangia maoni ya Utunzi wa Katiba mpya, kwa sababu kimetoa picha ya Makosa ya Msingi yaliyomo ndani ya Katiba iliyopo. Hivyo marekebisho yoyote ni lazima yachunge mtazamo huo.

Mola Atupe Tawfiq.
18/5/1432 H sawa na 22/4/2011 M
Shekh amemalizia hapo.

Ndugu zangu maulamaa wetu wamefanya jitihada ya kuwasilisha haya kama muongozo, sasa kazi inabakia kwetu kama wawakilishi ama wasemaji wa upande mwingine nakusdia wasomi wa chuo.

IMEWASILISHWA KATIKA BLOG YA UDOMSA TAREHE 9/04/2011
RABBANA AATINA FII DUNIYA HASANA, WAFIL AAKHERAT HASANA, WAAKINAADHAABA-NNAR

Wednesday 13 April 2011

MAKALA MUHIMU KUZIJUA

Bismillah.
FUNGUENI- KWANINI TUNAOGA JANABA
                      KWANINI MANII SIO NAJISI?
                     

KWANINI UISLAMU UMERUHUSU KUOA MKE ZAIDI YA MMOJA?.

Swali hili twaweza liuliza hivi: Kwanini wanawake hawafai kuolewa na mume zaidi ya mmoja,ila wanaume wamepewa ruksa ya wake wanne?
Hili linabainishwa kwa aya ya mwenyezimung ifuatayo:

[Anisaa:3]
“Na ikiwa mnaogopa kuwa hamtowafanyia mayatima uadilifu, basi oeni mnao wapenda katika wanawake, wawili au watatu au wane. na mkiogopa kuwa hamwezi kufanya uadilifu, basi mmoja tu, au wale ambao mikono yenu ya kulia imewamiliki. Kufanya hivi ndiko kutapelekea msikithirishe wana”.
ALLAH ameruhusu mwanaume kuoa mke zaidi ya Mmoja na si mwanamke kuolewa na mwanamme zaidi ya mmoja kwani yeye(mwanamke )anahifadhi bacteria na virusi vinavyojengeka na mwili wa mwanadamu wapatikanao katika manii ya mwanaume na hivyo kimaumbile akihifadhi bacteria na virusi vya zaidi ya mwanamme mmoja ataleta madahara yafuatayo:
1. Ataleta mapiganao aya viumbe bacteria katika mfumo wake wa uzazi ulio na tabia ya kimaumbile kuyapokea na kuayahifadhi kupitia mfumo wake wa uzazi bacteria hawa ni pamoja na mjengo acidi uoneshao asili ya mwanadamu na kitambulisho cha mtu uitwao DNA(Deoxyribonucleic Acid) utaokanao na kujengwa na damu,mate na mbegu za kiume za mwanadamu. Bacteria hawa wakipigana hufa miongoni mwao kuleta uozo ujengao Neisseria gonorrhoeae na wengine hujengwa waitwao Chlamydia trachomatis, Treponema pallidum ,hukimbilia katika sehemu ya ndani ya mfumo wa uzazi kupitia nyama laini inayoujenga mfumo huo hivyo kuleta MAGONJWA kama klamadia,kaswende,kisonono na maumivu, hali hii na athari zake hujijenga na kuwa mabaya zaidi endapo itakuwa mapigano ya bacteria wa namna tofautitofauti kutokana na mwanamke kushiriki jimai na wanaume wengi.

2. Pia kutapatika muingiliano baina ya virusi mwili na kuzaliwa/ kujengwa virusi wapya wenye madhara waitwao kitaalamu herpes simplex virus(HSV) wasababishao ugonjwa wa malengelenge na hatari zaidi ni kupatiakana kwa Human immunodeficiency virus (HIV) washambuliao kingamwili.

Kulazimika kwa ndoa katika uislamu kuna hekma kubwa ambayo huyaepusha haya na pia kuyaepusha haya Allah (sw) amewalazimisha wanawake na wanaume kudumu katika jimai ya ndani ya ndoa. Mwanamke anapokea viambato vya mwanaume mmoja tu kwa namna ya maumbile aliyowaumbia Allah (sw) na sikinyume na hapo, kuyaasi haya ndipo zinakuja adhabu za mungu zinazotibika na zisizo na tiba kama UKIMWI.
Wataalamu wanasemaje katika uwezo wa uzalishaji na haja ya jimai:
Mwanaume wakawaida mwenye nguvu, mzima wa mfumo wa uzazi ana uwezo wa kuwahudumia wanawake watatu hadi wane kwa haja zote mbili za kuwatosheleza kwa mahitajio na akshi za kimwili pia kwa majenzi ya uzazi na kuzaliana, kwani wanaume wameumbiwa uwezo wa kutengeneza mbegu na mshindo wa jimai zaidi kuliko wanawake.

Wednesday 6 April 2011

NA KHALID BILAL
Assalaam alykum,
Hivi karibuni kumezuka tiba ya ajabu ambayo imewashangaza wengi kitaifa na hata kimataifa, tiba hiyo ambayo ipo kiimani zaidi kutokana na madai ya hao wanaotoa tiba hiyo kudai kuwa wameoteshwa na Mungu/bikira maria/krsito/mizimu pia kufanikiwa kwa tiba hiyo kunategemea na imani ya mtu juu ya tiba hiyo kuwa inaponya, pia wanadai kuwa tiba hii inatibu magonjwa sugu ya aina yoyote kama vile kansa, presha, kisukari, ukimwi na mengineyo.
Cha kushangaza zaidi juu ya tiba hii ni juu ya asili ya tiba hiyo na kwamba tiba hii haina dozi, ni kikombe kimoja mpaka viwili na ugonjwa wako huondoka lakini pia tiba hii hupatikana kwa kuchemshwa mmea ambao kwa baadhi ya jamii mmea huo hujulikana kama ni sumu.
Nao watanzania wajikuta wanaipokea tiba hii moja kwa moja bila kujiuliza na kufikiria kwa umakini ukweli na undani wa tiba hii, kuna baadhi ya waliopata tiba hiyo wanadai wamepona na wengine wanadai bado hawajapona. Nayo serikali ya Tanzania yaingilia mambo ya kiimani na baadhi yao kupelekea kuingiliana katika majukumu ya uongozi pia viongozi wa dini nao hawakuwa nyuma katika hili. Haya yote si kwamba nimeyatoa kichwani bali ni kupitia ushahidi wa magazeti mbalimbali na usikilizaji wa redio. Ngoja tuanze kujua undani wa:
TIBA YA BABU LOLIONDO
Mchungaji Mstaafu wa KKKT (Babu), Ambilikile Mwasapile, umri (78) aishie kijiji cha Samunge, Loliondo, wilaya ya Ngorongoro, mkoa wa Arusha. Ni mchungaji mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini na Kati, ambapo alitumikia utumishi huo kwa kipindi cha zaidi ya miaka 20, alifanya kazi hiyo kwa uadilifu uliotukuka na kazi yake imekuwa mfano wa kuigwa na wengine mpaka leo. Mchungaji huyu mstaafu alianza kutoa tiba ya kikombe Agosti 2010 huku akisema hadharani wala hakusema kwa siri kuwa dawa yake imepata uponyaji wa kimungu, kwa maana kuwa kinachoponya sio ile dawa bali ni neno la Mungu kwenye ile dawa. (Gazeti la Tanzania daima 30-03-2011)
Mchungaji huyo alisema “Nimefanya kazi za uchungaji tangu mwaka 1967 katika sehemu kadhaa nchini hadi mwaka 1989 nilipohamishiwa katika eneo hilo. Na nimefanya kazi za uchungaji hapa hadi nilipostaafu mwaka 2002”. (Gazeti la Raia mwema 16-03-11)
Pia alisema “Nilianza kuota maono na kusikia sauti ya Mungu tangu mwaka 1991 ikinieleza kuwa nibaki kuishi eneo hili; kwani Mungu alikuwa anataka kunipa kazi maalumu ambayo kwa wakati huo sikuifahamu” (Gazeti la Raia Mwema toleo 176)
Mchungaji Mwasapile amewaambia waandishi kwamba dawa hiyo alionyeshwa na Mungu, na kwamba yeye anakawaida ya kuzungumza na Mungu mara kwa mara. Anadai pia kwamba Mungu ndiye aliyemwambia kwamba aitoze TSh.500/= kwa kila mgonjwa anatakayempa kikombe cha dawa hiyo ambayo ni ya kikombe kimoja cha maji yaliyochemshwa ya mizizi ya mti unaoitwa mugariga au muugamuryaga (kwa lugha ya Kisonjo). Na magonjwa anayotibu ukimwi, kisukari, saratani, kansa, , shinikizo la damu (presha), kifafa na magonjwa mengine sugu ambayo yamekuwa yakitishia uhai wa maisha ya Watanzania wengi.(Gazeti la Raia Mwema 22-03-11)
KHALID: Hapa ni wazi kuwa tunataka tubadilishwe imani zetu bila ya wenyewe kujua, hakuna mwenye uwezo wa kuzungumza na Mungu isipokuwa Mitume na Manabii nao wameshaisha/wameshafariki, Je huyu ni Mtume/Nabii au TAPELI? Huu ni mpango wa kanisa katika kutufanya tumshirikishe Mungu, yani tuwe WASHIRIKINA.
Inaendelea, Gharama ya tiba hiyo ni Tsh 500/= ambapo Tsh 200/= ni kwa ajili ya kanisa, Tsh 200/= kwa ajili ya kuwalipa wafanyakazi wake na 100/= ndo yake binafsi, Lakini hata hiyo, Sh 100 ambayo inakwenda kwake haitumii, kwa sababu anasema kila kitu kuhusiana na dawa hiyo ni kwa mujibu wa maono aliyopewa na Mungu, hivyo hata hizo Tsh100/= hatazitumia hadi pale Mungu atakapompa maelekezo. Ni mti huo huo unaotumiwa na Babu wa Loliondo kuponya ambao Wagogo wao huutumia kama sumu kwenye mishale yao; wenyewe wanauita “usungu”! (Gazeti la Raia Mwema 30-03-2011)
Baadhi ya majina ya mmea wa babu ni pamoja na angelica archangelica, na jina jingine linalorushwa ni mmea wa Carissa edulis na jina ambalo limetushtua wengine ni lile la mmea wa antiaris toxicana. Mimea yote hiyo mitatu ina sifa za madawa.
Mmea wa Carisa edulis - nao una sifa kadha wa kadha za kimadawa Kuanzia mzizi, magamba na majani yake yote yana sifa ya kutumika kimadawa. Na umetumika sehemu nyingi duniani kama tiba vile vile, Baadhi ya sifa zake nayo ni kutumika kupunguza maumivu. Unaweza pia kusaidia kutibu saratani na magonjwa mengine.
Mmea wa angelica archangelica - unajulikana sehemu mbalimbali duniani kutumika katika tiba za mitishamba, na watu kadhaa katika historia wamewahi kudai kuoteshwa ndoto juu yake ili wautumie kwa ajili ya uponyaji tangu karne ya 12, Baadhi ya sifa zake za kitabibu ni pamoja na kupunguza maumivu, na kusisimua mfumo wa kinga za mwili na hata kushambulia maambukizi ya bakteria na virusi.
Mmea wa antiaris toxicana - huu hujulikana kama mkuki wa sumu. Unajulikana hivyo kwa sababu tangu kale sumu yake imekuwa ikitumiwa kuweka kwenye mikuki na mishale kwa ajili ya mapigano na inadaiwa ni sumu kali sana. (Gazeti la New Habari 21-03-11)
Babu amesikika akisema yafuatayo, kuna watu ambao wameanza kuwaambia vijana wa huku kwetu ambao wanajua miti hiyo tunayoitumia kwamba wawachimbie, na wapo ambao wameshachimbiwa tayari kwa lengo la kwenda kutengeneza dawa. Akaendelea kusema:
“Sasa nawambia ya kwamba si kweli, huo ni wizi sikubali mtu yoyote mahali popote kupewa dawa na mtu kwamba mimi nimeitambua dawa hiyo, Mungu hakuagiza hivyo, naomba taifa letu lijaribu kuwatangazia mataifa mengine kuwa dawa ya aina hiyo haitakuwa dawa, hadi pale Mungu atakapoagiza vinginevyo.
“Kwa wakati huu amemruhusu mtu mmoja tu ambaye ni mimi kutoa dawa hii, nitakapochimba dawa hiyo na mwingine akachimba, Mungu ameniambia kuwa ya huyo mtu si dawa, kwa hiyo watu wasidanganywe na matapeli”
“Kuhusu masharti ya dawa hakuna, ila mimi nimeweka sharti moja, si Mungu, nawaambia watu kwamba ukitumia dawa hii basi kama wewe ni mtumiaji wa pombe usinywe siku uliyokunywa dawa na kama sharti hili lisingekuwa sawa, basi Mungu angeniambia.”
“Nimesema hivi dawa nnayotoa ina nguvu za Mungu, kwa hiyo inashika pahala pa dawa alizokuwa akitumia mgonjwa, sasa ni hiari ya mtu kuendelea kuzitumia au kuziacha. Pia dawa hii inatibu kila ugonjwa maana watu wameniletea taarifa walipopona ugonjwa fulani,wamesema hata magonjwa mengine waliyokuwa nayo yamepona, lakini pamoja na hayo sio kinga, ni ya kutibu aje mtu ambaye ni mgonjwa anaumwa”. (Gazeti la New Habari 21-03-2011)
KHALID: Mbona mambo mengine anajiamulia yeye mwenyewe bila ya kuambiwa na Mungu? Kama tiba ni mti na si imani mbona anawazuia watu wasiutumie? Hapa ASITUDANGANYE, tiba hii ni ya imani ya kikristo na si mti, hivyo tukimfuata tutakuwa tumefanya shirki tena shirki kubwa.
Ngoja tupate majibu ya baadhi ya wagonjwa walokunywa kikombe cha babu, baadhi walisema wamepona na baadhi waliyasema haya;
“Bado sijisikii vizuri ila naomba usiandike mambo yangu kwenye magazeti….dawa niliyokunywa ilifanya kazi kwa siku mbili tu na baada ya hapo ugonjwa umeendelea kama kawaida,” alieleza mgonjwa huyo kwa kifupi akiwa katika hospitali hiyo binafsi (jina limehifadhiwa)
“Bado ugonjwa unaniandama ndugu yangu. Sijapata nafuu yoyote na dawa niliyokunywa Loliondo haijanisadia hata kidogo…..nimeona niendelee tu na matibabu ya hospitali kama nilivyokuwa nafanya awali,” alisema mgonjwa anayeishi Mombo mkoa wa Tanga mwenye asili ya uarabu
“Ukweli ni kwamba bado nina virusi baada ya kufanyiwa vipimo katika hospitali ya Selian. Bado virusi vipo. Nilikuwa nataka kurudi Loliondo nikanywe dawa kwa mara ya pili lakini nimeambiwa tiba ya Babu ni mara moja na hairudiwi tena,” alisema mgonjwa wa ukimwi (jina linahifadhiwa) (Gazeti la Raia Mwema 22-03-2011)
Sasa ngoja tujue nini kilichotokea baada ya viongozi wa dini wa KKKT na wengineo walichokifanya juu ya uendeshwaji na utolewaji wa tiba hii ya kikombe ya Mchungaji Mstaafu:
NI Agosti 25 mwaka 1989 katika ukumbi wa mikutano wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) ulioko Oldonyosambu wilayani Arumeru ambako wachungaji 103 wa Kanisa hilo wamekutana wakimsubiri Askofu Mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini na Kati, Thomas Laizer.
Walikuwa wanakutana kumchagua Mchungaji atakaye kwenda kuziba pengo lililoachwa wazi na Mchungaji Simeone Kiserian wa usharika wa Sonjo mtaa wa Samunge ambaye alikuwa amefariki dunia.Wengi walitarajia suala hilo lingekuwa moja ya ajenda ngumu kutokana na watumishi wengi kutopendelea kwenda eneo hilo kufanya kazi ya kueneza injili kutokana na mazingira magumu ya kazi yaliyopo katika wilaya hiyo ya Ngorongoro.
Mchungaji aliyekubali kwenda kufanya kazi ya kueneza neno la Bwana hakuwa mwingine zaidi ya Mchungaji Ambilikile Mwasapile ambaye alijitokeza kwa hiari yake mwenyewe kuwa alikuwa tayari kwenda eneo hilo kufanya kazi na kuziba pengo lililoachwa wazi.
Ni Mchungaji huyo ambaye sasa ana miaka 78 na akiwa tayari amestaafu kazi tangu mwaka 2002 ndiye amekuwa gumzo kubwa nchini kwa kipindi cha mwezi mmoja sasa kutokana na madai kuwa amegundua dawa ya ajabu ambayo imekuwa inatibu maradhi sugu kama ukimwi, kansa, kisukari, pumu, shinikizo la damu na mengineyo.
Thomas Laizer na Maaskofu wenzake wawili wa Kanisa hilo na wajumbe wa watu 21 walikwenda Samunge kujionea tiba hiyo na baada ya kuridhika kuwa inatolewa kwa kufuata taratibu za Kikristo walikunywa dawa ya Mchungaji huyo na tayari wanajisikia nafuu baada ya kuinywa. Babu wa Liliondo ni kama vile Padri Nkwera, anafanya kazi ambayo kanisa na Serikali wameshindwa kufanya au hawana uwezo kuwafikia wagonjwa wote. (Gazeti la Raia Mwema 22-03-2011)
Kama hiyo haitoshi, Mchungaji Mwaisapile arudishwa kazini. Wakati Babu Mwasapile akizidi kuvuta watu, Kanisa lake la KKKT limemrudisha kazini kwa kumwongezea mkataba wa ajira usiyo na kikomo, ikiwa ni miaka minne baada ya kustaafu, hivyo kumwezesha kuendelea kupata mshahara na stahili zingine.
Ajira hiyo isiyo rasmi imetokea kwa mchungaji huyo mara baada ya kudaiwa kupata karama kutoka kwa Mwenyezi Mungu na kuanza kutibu magonjwa sugu yakiwemo kisukari, saratani na UKIMWI kwa kile kinachoelezwa kuwa tiba hiyo inafanyika kwa njia ya imani na kimaombi.
Kuajiriwa upya kwa mchungaji huyo kutamwezesha kupata mshahara kama kawaida na kusitisha pensheni aliyokuwa akiipata kama mchungaji mstaafu.
Askofu wa KKKT Dayosisi ya Kaskazini na Kati, Thomas Laiser alithibitisha kurudi kazini rasmi kwa mchungaji huyo jana, akisema kanisa hilo limetafakari na kubaini umuhimu wa mchungaji huyo katika dayosisi hiyo na taifa kwa ujumla, na kumrudisha ili atumikie umma akiwa ndani ya kanisa hilo.
Alisema mchungaji huyo alipewa kazi hiyo na Mwenyezi Mungu tena kazi kubwa kuliko hata ile aliyokuwa akiifanya kabla ya kustaafu, hivyo iwapo ametukuzwa na Mungu kiasi hicho vipi wao wasimjali na kumweka katika himaya ya kanisa.
Mchungaji Mwaisapile ambaye atabakia katika Usharika cha Sonjo alipokuwa akitumikia awali, alistaafu baada ya kulitumikia kanisa hilo katika maeneo mbalimbali, ukiwamo Ushariki wa Babati Mjini, Mkoa wa Manyara kwa miaka saba kabla ya kuhamia Sonjo alikotumikia kwa miaka 12 hadi kustaafu. (Gazeti la Majira 22-03-2011)
ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Moravian Tanzania, Alinikisa Cheyo amewaonya viongozi wa dini wanaojiita mabingwa wa uponyaji wanaoponda matibabu ya mchungaji Ambilikile Mwasapile wa Kijiji cha Samunge, Loliondo wilayani Ngorongoro na kuwataka kuacha tabia ya kukaa kwenye maombi ili Mungu awajibu. Alisema “nawambia ndugu zangu katika siku za sasa watu wamekuwa wakiamini sana habari ya Loliondo na kila leo kumekuwa na taarifa za Loliondo, mimi nasema kuwa kinachoponya ni imani ya mtu anayekwenda huko na bila imani atakuwa amepoteza muda kwani mchungaji Mwasapile anamtegemea Mungu”.
Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini Kati, Thomas Laiser amewataka wanaochonga juu ya tiba hiyo wafunge midomo yao badala ya kuzuia watu wasikimbilie huko. “Tunachoamini tiba hiyo ina mahusiano makubwa na imani na maombi, na katika maombi kuna kukubaliwa mapema, baadaye na maombi mengine kukataliwa kabisa. Mambo ya Kimungu ni ya Mungu ni vigumu kuyabadilisha kibinadamu, nimekuwa nikipata simu nyingi toka Rwanda, Uganda, Burudi na kwingineko kuom ba mchungaji Mwasapile kubadilisha kituo cha huduma, nawajibu kuwa haiwezekani kwani ni suala la kiimani na maombi hata mchungaji mwenyewe alipenda kutoa tiba hiyo Babati mkoani Manyara alikataliwa”alisisitiza Askofu Laiser. Askofu Thomas Laiser aliendelea kusisitiza kuwa kanisa hilo katika kuhakikisha azma yao inatimia linatarajia kutumia zaidi ya sh milioni 75 katika kuboresha mazingira ya tiba hiyo.
Huduma ya uponyaji inayoendeshwa na Babu imeendelea kuwachanganya baadhi ya viongozi wa dini, wa karibuni kabisa akiwa Mchungaji Christopher Mtikila ambaye ameiponda na kuwaponda waotumia dawa hiyo kutibu maradhi mbalimbali. Licha ya Mchungaji Mtikila kukiri mbele ya waandishi wa habari kuwa dawa hiyo inaponya, ameiponda na kudai kuwa hakuna jipya linaloendelea huko Loliondo. Mchungaji Mtikila jana alitoa mpya pale aliposema 'hata vikombe vinavyotolewa kunywea dawa hiyo ni vya rangi ya kijani na njano, hivyo akadai kwamba hiyo ni zindiko la CCM'. Pia alisema kwamba Loliondo hakuna neno la Mungu, bali ni 'machemsho ambayo wananyeshwa watu bila imani katika Kristo'.
Kiongozi wa Full Gospel Bible Fellowship Askofu Zachary Kakobe wamekuwa wakitoa kauli mbalimbali za kupinga huduma hiyo inayokimbilia na maelfu ya watu wa ndani na nje ya nchi. Askofu Kakobe alivitaja vigezo vya kwenye Biblia takatifu vinavyoonyesha kuwa dawa hiyo si lolote. Kimojawapo kikiwa ni kwamba hakuna huduma ya Mungu ambayo hupangiwa bei! (Gazeti la Majira 21-03-2011)
KHALID: Mbona kanisa linamsimamia kidete Babu wa Loliondo na kuapa kuwa sambamba naye kwa hali na mali? Hii ni wazi kuwa suala la Babu ni la kidini, waislamu tusiwe wajinga wa kumkubali/kuikubali tiba yake kwa njia yoyote ile.
Kuwepo kwa sura kisiasa kulijitokeza wiki mbili zilizopita ambapo Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Haji Mponda alimwagiza Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Isidore Shirima kumzuia Mchungaji huyo kuendelea na tiba yake, lakini siku moja baadaye Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri Mkuu (Sera), Wiliam Lukuvi alitengua amri hiyo na kuagiza utoaji tiba uendelee kwa hoja kwamba suala hilo lilikuwa la kiimani zaidi.
KHALID: Ona viongozi ambao tumewapa madaraka ya kutuongoza wanavyoshabikia suala lisilo na mantiki na la kipumbavu. Hivi kiongozi kama huyu anaweza akaleta mabadiliko ya kweli kwenye jamii kama kuondoa ufisadi na rushwa? WAISLAMU TUWE MAKINI TUCHAGUAPO VIONGOZI.
Makamishna waandamizi na makamanda kadhaa wa Jeshi la Polisi nchini walitinga kwa babu kupata kikombe hicho.Viongozi hao wa jeshi hilo walipata fursa hiyo baada ya kumalizika kwa mkutano mkuu wa watendaji wa jeshi hilo uliofanyika Chuo cha Polisi Moshi hivyo wakaona watumie furasa hiyo kumfikia Babu kabla hawajarudi katika vituo vyao vya kazi. (22-03-11—majira)
KHALID: Hawa nao ni wana usalama katika jamii, Hivi wananchi tutakuwa salama kweli wakati tulowaweka kutulinda hawana usalama, hawafikiri na kuchunguza kabla ya kutenda? Kwa hakika wananchi hatuna budi tuchukue tahadhari za haraka juu ya viongozi wetu ama si hivyo tutaingizwa gizani(kwenye upotevu ulio mkubwa).
Ya Loliondo yanadhihirisha jinsi Watanzania tusivyopenda kuhangaisha akili zetu kufikiri. Sisi tu wavivu wa kufikiri, na wavivu wa kuchanganua mambo. Tumezoea njia za mkato hata kwenye masuala nyeti kama ya tiba. Na Babu wa Loliondo amekuwa njia ya mkato kwa wagonjwa wengi! Tafakari.
Nayo Serikali haikushighulisha kichwa ktk suala la loliondo, Mchungaji mstaafu wa KKKT, Ambilikile (Babu) alisema hadharani wala hakusema kwa siri kuwa dawa yake imepata uponyaji wa kimungu.Ni neno la Mungu ndilo linatibu. Tena akaeleza kuwa dawa yenyewe ameoteshwa katika ndoto na Mungu, hivyo akakiri kuwa dawa yake ni tofauti na dawa nyingine kwani dawa nyingine mgunduzi ni mwanadamu na zimefanyiwa utafiti, lakini hii ya Loliondo ni ya neno la Mungu lililomjia katika ndoto.
Tunukuu kauli ya serikali na wataalamu wake, “Serikali imesema imeridhishwa na dawa inayotolewa na Mchungaji Ambilikile Mwasapile wa Kijiji cha Samunge, Loliondo ikisema haina madhara yoyote kwa matumizi ya binadamu. Akitoa tamko la timu ya wanasayansi waliofanya uchunguzi wa awali wa tiba hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), Charys Ugullum, alisema timu hiyo ilianza utafiti wake wa awali Machi 7, mwaka huu. Alisema timu hiyo ilijumuisha wataalamu kutoka Wizara ya Afya, TFDA, Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Mkemia Mkuu wa Serikali na Taasisi ya Utafiti wa Dawa za Asili ya Chuo Kikuu cha Afya ya Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS).
Katika suala hili kwanza serikali imechelewa kutoa tamko, kama dawa hiyo ingekuwa na madhara kwa wanadamu wangapi wangeathirka, na kwanini serikali ilisubiri muda mrefu wote mpaka karibu viongozi wote wa serikali wamekunywa ndipo inatoa tamko. Ni uzembe au kutokuwa makini?
Hivi wasomi hawa wote hawakufikiri hata mara moja kuwa ni ujinga kupima kitu kilichosemwa ni neno la Mungu kwa kutumia vifaa vya maabara?. Tangu lini na wapi ndoto zinapimwa kwa kutumia vifaa vya maabara, Mkemia Mkuu anajua nini kuhusu Elimu ya ndoto?. Dawa inayosemekana inatoka kwa Mungu, inayolingana dozi kwa kila ugonjwa, inayohusisha imani kabisa bila nguvu za kisayansi, kweli serikali ilipaswa kutenga pesa kutafiti kama neno la Mungu linatibu? Serikali yenyewe ingemwona wapi Mungu na kuuliza nguvu ya uponyaji ya huo mti uliokuwepo katika mazingira hayo kila siku?
Serikali bila aibu inasema, “tena kinachofuata sasa tutachunguza kama kweli dawa hiyo inatibu magonjwa hayo matano aliyoyasema Babu. Hivyo wananchi wawe na subira ili watupe nafasi tufanye utafiti wa kina zaidi.” Je, ikitokea kuwa dawa hiyo haitibu watachukua hatua gani?

Mkurugenzi wa Uendelezaji na Uratibu Utafiti kutoka Tume ya Sayansi na Teknolojia, Dk. Rose Kingamkono akasema wanafuatilia ili waweze kujua kama kuna hatimiliki ya tiba hiyo. Aliendelea kusema “Wananchi wasitoe mbegu au mti huo ovyoovyo maana wajanja wanaweza wakauchukua kwenda kutengeneza dawa kisha kuja kutuuzia tena kwa gharama kubwa.” Jamani viongozi wa serikali yetu wanafikiri sawa sawa? Mti upo porini, inasemekana umetiwa nguvu ya uponyaji na Mungu kwa kupitia mchungaji Mwasapile, wala si mtu mwingine, ndiyo maana hata wataaalamu hao wa tiba hadi sasa hawajachukua mizizi kupeleka Muhimbili, Bugando au KCMC kutibu wagonjwa, iweje mtu afikirie neno la Mungu kuwekewa hatimiliki, na kuzuia nguvu ya utendaji au uponyaji wa Kimungu usiende kwingine? Je, mtu mwingine akiota Kenya leo, Uganda kesho na Uturuki wiki ijayo na kupewa uwezo kama wa Mwasapile, serikali yetu itazuia huduma za ndoto za Kimungu katika mataifa mengine kwa kuwa mtanzania ndio alikuwa wa kwanza kuota ndoto na kupewa maelekezo na Mungu?
Msajili wa Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala, Dk. Paulo Mhame alisema hivi sasa wako katika hatua za mwisho za kumpatia cheti cha usajili Mchungaji Mwasapile. Wanampatia kama mganga wa jadi kwa utaratibu upi?
NDUGU ZANGU TUCHUKUE TAHADHARI JUU YA VIONGOZI WETU, WANATUDHALILISHA KWA MAMBO WANAYOYAFANYA, MBONA HAWASHUGHULISHI VICHWA VYAO. VIONGOZI WENYEWE WANAOHIMIZA KUWEPO KWA TIBA HII WOTE NI WAKRISTO HIVYO TUJUWE WAZI KUWA HAPA KUNA UDINI, PIA WANATETEANA ILI KUUENDELEZA UDINI WAO. WAISLAMU TUWAMKE TUGOMBEE KWA WINGI NAFASI ZA UONGOZI AMA SIVYO TUTARITADISHWA.
Namnkuu Paroko mmoja aliyetupa mawazo ya kujifikirisha kidogo kuwa "Sina chuki wala tatizo lolote na tiba ya Loliondo, lakini kama unataka kwenda lazima ujiulize maswali manne yafuatayo:
Kwanza, tiba inayotokana na miujiza ya Mungu lazima iwe endelevu, isiwepo kwa kipindi kifupi tu.
Pili, watu wajiulize kama miujiza kutoka kwa Mungu huwa na masharti?
Tatu, wajiulize kama tiba hiyo inafanya kazi ndani ya Loliondo, kwanini isifanye kazi Dar es Salaam na kwingineko?
Nne, wajiulize kuhusu tiba hiyo ya magonjwa sugu ukiwemo ukimwi, je, Mungu aliwaumba wanadamu na kisha kuamua kuwaangamiza? Au wanadamu wanaangamia kutokana na vitendo vyao vya ujanja ujanja?” (Gazeti la Tanzania daima 30-03-2011)
Hao ndo yale yalojiri kutokana na tiba ya Mchungaji Mstaafu Ambilikile Mwasapile maarufu kwa jina la ‘Babu’ wa Loliondo. Nao wengine wajitokeza kutoa huduma ya tiba ya kikombe katika sehemu mbalimbali nchini Tanzania, pata hii;
TIBA YA KIKOMBE ROMBO
KUTOKANA na kujitokeza kwa mtu mwingine wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro anayetoa dawa ya kutibu magonjwa sugu kama alivyo Mchungaji mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwaisapile 'Babu', mtu huyo amesitishwa na Ofisa Mtendaji wa Kata kuendelea na huduma hiyo.
Akizungumza na gazeti hili kwa simu, kijana huyo aliyejitambulisha kwa jina la Hilali James, umri (28), alisema endapo Serikali itashikilia msimamo wake wa kuendelea kuisitisha huduma yake, tayari ameoteshwa ndoto kuwa atatokea mtu mwingine ambaye ataendelea kuitoa huduma hiyo.
James alisema huduma hiyo alikuwa akiitoa katika Kijiji cha Mbomani Chini Kata ya Tarakea wilayani Rombo, ambapo masharti yake ni mtu kutakiwa kunywa vikombe viwili kwa wakati mmoja na hairuhusiwi kurudia.
Mbali na kunywa, alisema alioteshwa ndoto kuwa atapokea Sh 500/=, ambazo kati ya hizo, Sh 200/= ni kwa ajili ya matumizi yake ya kuwalipa wafanyakazi, na Sh 300/= za kuwasaidia yatima na watu wasiojiweza. Akizungumzia magonjwa yanayotibiwa na dawa yake, alidai inatibu shinikizo la damu, kisukari pumu, saratani, figo, Ukimwi na magonjwa ya tumbo. Pia alidai tayari watu wapatao 100 wamekwisha inywa dawa hiyo na kupata uponyaji.
Kijana huyo mwenye mke na watoto wanne, alibainisha kuwa awali alikuwa fundi wa baiskeli, na kwamba chanzo cha kuanza kutoa dawa hiyo ni kutokana na kuoteshwa ndoto na Yesu Kristo usiku na mchana. Alisema mti aliooteshwa kuutumia hadi sasa hajaufahamu jina lake, na kuwa ulikuja katika ndoto na hajawahi kuuona tangu kuzaliwa kwake.
Alisema yeye kuibuka baada ya Mchungaji Mwaisapile si tatizo kwa sababu, kila jambo lina wakati wake, hivyo wakati huu ni wake. (21-03-11 Habari Leo)


KHALID: Ndugu zangu waislamu tufumbuke macho. Mbona hizi tiba zote asili yake ni ndoto tu hamna hata maandiko!? Mbona tunataka tubabaishwe na watu wanaoota?! Hivi wangapi mpaka leo wanaota, je wakiamua kutangaza ndoto waotazo itakuaje? Ndugu yangu umizwa kichwa katika kila tukio litokealo ili kujua undani wa tukio hilo na si kukurupuka na kuchukua maamuzi yasiyo na msingi.
TIBA YA KIKOMBE MBEYA
SERIKALI Mkoa wa Mbeya jana ilisalimu amri kwa mganga aliyeibuka akitibu magonjwa mbalimbali, Jafari Welino, umri (17) na kujikuta ikibariki huduma baada ya wagonjwa wanaotegemea huduma hiyo kuandamana na kutishia kulipua Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.
Akijibu maswali kijana huyo aliyeonekana mwenye ujasiri alisema kuwa yeye alipewa kazi hiyo baada ya kutokewa na mzimu (wa mama yake mzazi) katika usingizi/ndoto ambapo alikatazwa kusoma shule na kuoneshwa mti ambao aliambiwa kuwa utakuwa ukombozi kwa watu kwa kuwapa vikombe viwili kwa siku mbili bila ya malipo.
Taarifa ya awali iliyolifikia gazeti la majira la tarehe 29-03-2011 (soma uk. 9) ilisema kuwa Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ilikuwa imemzuia kijana huyo kutoa huduma ya tiba kwa madai kuwa mazingira ya utoaji wa huduma hiyo ni machafu na kuwa dawa anayotumia ilitakiwa ifanyiwe uchunguzi ili kuona kama ni kweli inaweza kuponya magonjwa sugu bila kuleta madhara kwa afya za binadamu.
Kutokana na hali hiyo, baada ya wagonjwa waliokuwa wamefika nyumbani kwa kijana huyo eneo la Mabatini, kilomita 2.5 kutoka katikati ya Jiji la Mbeya wakiwa na vikombe mikononi walikubalina kuandamana kwenda kwa mkuu wa Mkoa wa Mbeya.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Bw. John Mwakipesile alitoa amri kwa kijana huyo kuendelea kutoa huduma huku idara zinazohusika zikifuatilia kuona namna ambayo itafanya, ili kijana huyo aweze kutoa huduma katika hali ya usafi wakati utafiti wa dawa hizo ukiendelea.Katibu Tawala Msaidizi Bw. Chitama alisema kuwa serikali haina ugomvi na waganga wala imani za dini, na hivyo kinachotakiwa kwa kijana huyo ni kuhakikisha anafanya kazi hizo katika mazingira safi ili kutoathiri afya za wagonjwa wake.
Kuhusu kuhama katika eneo hilo, alisema kuwa hawezi kufanya hivyo kwa agizo la serikali badala yake anasubiri mizimu yake iweze kumweleza jambo hilo na sehemu ya kwenda na ndipo atakapoamua kufanya hivyo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Bw. Advocate Nyombi alisema yeye anachoangalia ni hali ya usalama wa watu wanaomiminika katika eno hilo dogo kupata huduma, huku akitaka mamlaka nyingine zifanye kazi yake ili kudhibiti uvunjifu wa amani unaoweza kutokea. (Gazeti la Majira 29-03-2011)
KHALID: Sasa basi inatosha, mnataka mpaka mizimu nayo tuiamini? Hakika hii ni shirki kubwa tena ilo wazi kabisa na atakayemshirikisha Mwenyezi Mungu na kitu chochote atakuwa amepotea upotevu ulo mkubwa kabisa. Hivi kwa nini hawa viongozi wetu wa nchi wenye dini isiyokuwa ya kiislamu wanazikubali tiba hizi? Bila shaka si bure ndugu zangu wa kiislamu WANATAKA TUFUATE MILA ISIYOKUWA YA KIISLAMU.


TIBA YA KIKOMBE TABORA
Tiba hii inatolewa na Magreeth mutalemwa, umri miaka (40) mkazi wa Tabora, alianza kutoa huduma hiyo tangu tarehe 21-03-2011. Pia alisema “Nilikuwa nikipata msukumo baada ya kuoteshwa kabla ya tarehe 21 na kuidharau ndoto ile nilianza kupata matatizo lakini baada ya kuanza kufanya yale niliyotakiwa kufanya matatizo yakaisha ndio mpaka leo natibu watu”
Pia aliwazungumzi wenzake ambao wanatoa tiba kama yake kwa kusema yafuatayo “Ah ninavyoona mimi huu ni uwezo wa Mwenyezi Mungu tu, kwani katika uoteshwaji wangu nakumbuka sauti iliniambia tupo watatu na tumetunukiwa roho safi kufanya shughuli hii ya kutoa tiba. Kwa hiyo naamini hao ni wawili na mimi ni wa tatu na ndio tuliotunukiwa”. (keronyingi.blogspot.com tarehe 29-03-2011)
Waandishi wa Dar Leo walishuhudia viongozi wa vituo vikuu vya afya wakifika katika eneo analotoa dawa mwanamke huyo na kuchukua sampuli ya dawa hiyo.Wakati hayo yakiendelea mwanamke huyo Magreth Mutalemwa ambaye anatoa dawa hiyo kwa njia ya maombi kwanza amesema kuwa, anasikitishwa na baadhi ya wajanja ambao wamekuwa wakifika kwa nia ya kumjaribu kwa njia ya ushirikina.
Amesema kuwa, amekuwa akipata majaribu mara kwa mara tangu aanze kutoa tiba hiyo lakini kwakuwa anatumia zaidi imani ya kidini wachawi hao wamekuwa wakishindwa kutekeleza azma yao.Hata hivyo wakati wizara hiyo ikitoa tamko hilo mamia ya wakazi wa mkoa huo pamoja na vitongoji vya jirani wamekuwa wakiendelea kufurika kupata tiba kwa mwanamke huyo.Kutokana na hali hiyo Kamanda wa Polisi Mkoa huo, Liberatus Barlow amemwaga askari wa mkoa huo katika eneo hilo ili kuimarisha ulinzi. (Gazeti la Dar Leo 31-03-2011)
KHALID: Ndugu zangu katika imani, hapa hamna tiba bali ni Uchawi, Ushirikina, Utapeli/Ulaghai na Udini ndo unatawala. WAISLAMU TUSIKUBALI KUBABAISHWA NA YOYOTE YULE.

Haya ndo yale yalojiri katika tiba hii ya kikombe mpaka leo tarehe 02-04-2011nimeandika, ambayo inatibu aina zote za magonjwa sugu uzijuazo, lakini nikiwa kama muislamu, inanilazimu mimi na wewe uliyesoma makala hii KUKUTAHADHARISHA NA KUMTAHADHARISHA NDUGUYO MUISLAMU JUU YA TIBA HII YENYE SHIRKI NDANI YAKE. Katika mafundisho ya kiislamu tumefundishwa yafuatayo;-
 Hadithi ya Mtume (S.A.W), Kutoka Abu Huraira(R.A) Hakika Mtume (S.A.W) amesema “Yoyote atakayemuendea mpiga ramli / kuhani(ambaye mashetani wamemfundisha) akamuuliza jambo na akamsadikisha kwa yale aloambiwa na kuhani basi atakuwa amekufuru/amekanusha yale alokuja nayo Mtume (S.A.W)” Imepokelewa na watu wa Sunnah na Hakim
 Kutoka kwa baadhi ya wake za Mtume(S.A.W) kutoka kwa Mtume (S.A.W) amesema “Atakayemuendea Mpiga ramli na akmuuliza juu ya jambo, haitokubaliwa sala yako siku arobaini” Sahih Muslim
 Kama ukifuatilia kwa undani utagundua kuwa hamna tiba yoyote ni uzushi, uongo na ni propaganda za wasiokuwa waislamu kutaka kuwatawala watu kifikra. Allah (S.W) anasema katika Qur’an tukufu:-
 “Hiki ni Kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake; ni uwongofu kwa wachamungu”.(Qur’an 02:02)
 “Wala msiseme uwongo, kwa kuropokwa na ndimi zenu: Hichi halali, na hichi haramu - mkimzulia uwongo Mwenyezi Mungu. Hakika wanao mzulia uwongo Mwenyezi Mungu hawatafanikiwa”
(Qur 16:116)
 “Enyi mlio amini! Akikujieni mpotovu na khabari yoyote, ichunguzeni, msije mkawasibu watu kwa kutojua, na mkawa tena wenye kujuta kwa mliyoyatenda” (Qur’an 49:06)
Kwa maana “Enyi mlioamini! Akikujieni mtu ambaye yuko nje ya sharia ya Mwenyezi Mungu akakupeni khabari yoyote, basi chungueni mjue ukweli wake, kwa kuchelea msije mkawaletea watu madhara, kwa kutojua hali yao. Hapo tena baada ya kwisha dhihiri kuwa hawana makosa mkaingia katika majuto ya daima, mkatamani yasingeli kuwa.”
 “Wanataka kuizima nuru ya Mwenyezi Mungu kwa vinywa vyao. Na Mwenyezi Mungu atakamilisha nuru yake ijapo kuwa makafiri watachukia(8). Yeye ndiye aliyemtuma Mtume wake kwa uwongofu na Dini ya haki ili ipate kuzishinda dini zote, ijapo kuwa washirikina watachukia(9)”. (Qur’an 61:08-09)
 “Wala msichanganye kweli na uwongo na mkaificha kweli nanyi mnajua.” (Qur’an 02:42)
Kwa maana kuwa “Wala msichanganye Haki iliyo toka kwangu na upotovu mlio uzua nyinyi, hata ikawa halijuulikani la kweli na la uwongo. Wala msiifiche Haki, na katika hiyo Haki ni kumsadiki Muhammad, na nyinyi mnajua kuwa yeye ni wa kweli na wa kusadikiwa”
 “Enyi mlio amini! Msiwafanye wasiri wenu watu wasio kuwa katika nyinyi. Hawataacha kukufanyieni ubaya. Wanayapenda yanayo kudhuruni. Imekwisha fichuka chuki yao katika midomo yao. Na yanayo ficha vifua vyao ni makubwa zaidi. Tumekwisha kubainishieni Ishara ikiwa nyinyi mtayatia akilini”
(Qur’an 03:118)
 “Mayahudi hawawi radhi nawe, wala Wakristo, mpaka ufuate mila yao. Sema: Hakika uwongofu wa Mwenyezi Mungu ndio uwongofu. Na kama ukifuata matamanio yao baada ya ujuzi ulio kwisha kujia, hutapata mlinzi wala msaidizi kwa Mwenyezi Mungu” (Qur’an 02:120)
 “Mwenyezi Mungu, na Malaika, na wenye ilimu, wameshuhudia kuwa hakika hapana mungu ila Yeye, ndiye Mwenye kusimamisha uadilifu; hapana mungu ila Yeye Mwenye nguvu na Mwenye hikima(18). Bila ya shaka Dini mbele ya Mwenyezi Mungu ni Uislamu. Na walio pewa Kitabu hawakukhitalifiana ila baada ya kuwajia ujuzi, kwa sababu ya uhasidi ulio kuwa baina yao. Na anaye zikataa Ishara za Mwenyezi Mungu basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wa kuhisabu(19).” (Qur’an 03:18-19)
 “Hakika wanaouza ahadi ya Mwenyezi Mungu na viapo vyao thamani ndogo, hao hawatakuwa na sehemu ya kheri yoyote katika Akhera, wala Mwenyezi Mungu hatasema nao wala hatawatazama Siku ya Kiyama, wala hatawatakasa, nao watapata adhabu chungu(77). Na wapo baadhi yao wanao pindua ndimi zao katika kusoma Kitabu ili mdhanie kuwa hayo yanatoka Kitabuni, na wala hayatoki Kitabuni. Na husema: Haya yametoka kwa Mwenyezi Mungu. Na wala hayatoki kwa Mwenyezi Mungu. Na wanamsingizia Mwenyezi Mungu uwongo na wao wanajua(78).” (Qur’an 03:77-78)
 “Hakika wale walio kufuru baada ya kuamini kwao, kisha wakazidi kukufuru, toba yao haitakubaliwa, na hao ndio walio potea(90). Hakika wale waliokufuru, na wakafa hali ni makafiri haitakubaliwa kutoka kwa yeyote wao fidia ya dhahabu ya kujaza dunia nzima lau wangeliitoa. Hao watapata adhabu chungu, wala hawatakuwa na wa kuwanusuru(91)”. (Qur’an 03:90-91)
 “Enyi mlioamini! Mcheni Mwenyezi Mungu kama ipasavyo kumcha; wala msife ila nanyi ni Waislamu(102). Na shikamaneni kwa Kamba ya Mwenyezi Mungu nyote pamoja, wala msifarikiane. Na kumbukeni neema ya Mwenyezi Mungu iliyo juu yenu: vile mlivyo kuwa nyinyi kwa nyinyi maadui naye akaziunganisha nyoyo zenu; kwa neema yake mkawa ndugu. Na mlikuwa ukingoni mwa shimo la Moto, naye akakuokoeni nalo. Namna hivi Mwenyezi Mungu anakubainishieni Ishara zake ili mpate kuongoka(103)” (Qur’an 03:102-103)
 “Enyi mlioamini! Ikiwa mtawat'ii waliokufuru watakurudisheni nyuma, na hapo mtageuka kuwa wenye kukhasiri(149). Bali Mwenyezi Mungu ndiye Mlinzi wenu, naye ndiye bora wa wasaidizi(150).” (Qur’an 03:149-150)
 “Hakika Mwenyezi Mungu hasamehe kushirikishwa, na husamehe yaliyo duni ya hilo kwa amtakaye. Na anaye mshirikisha Mwenyezi Mungu basi hakika amezua dhambi kubwa” (Qur’an 04:48)
Pia Muislamu kuwa makini kwa kila tukio linalotokea dunia na hasa yale ambayo yanatokea kwa wasiokuwa waislamu kwani Allah(S.W) anatuhaikishia ktk Qur’an kuwa wasiokuwa waislamu hawana mapenzi/urafiki/nia njema na waislamu, lengo lao ni kuwabadilisha waislam na kuwafanya wafuate mila za wasiokuwa waislamu.
Allah(S.W) ndo mjuzi zaidi.
MUISLAMU CHUKUA TAHADHARI KWA KUTOISADIKISHA TIBA HII

NB: Kuwa makini pindi usomapo kwenye maneno yalopigiwa mstari

ALLAH SHUHUDIA KUWA NIMEFIKISHA
HAKUNA MKAMILIFU ISIPOKUWA ALLAH (S.W)


Kwa ushauri, msaada, changamoto, mapendekezo, nyongeza katika kuupeleka mbele uislamu, tuwasiliane kwa 0713174345, 0762121619, khalidbilaly@bismillah.com, khalidbilaly@yahoo.com.

WABILLAHI TAWFIIQ