بسم الله الرحمن الرحيم


بسم الله الرحمن الرحيم

UDOMSA.

Wednesday 15 September 2010

WAJIBU WA MUISLAM.

  WAJIBU WA MUISLAM


   Kabla ya kujuwa wajibu wetu hatuna budi kujitambua sisi wenyewe kwanza. Hivyo ni lazima kujiuliza masuala matatu ya msingi yafuatayo:-
1          Kwanza:          Sisi nani na tumeletwa na nani??
2          Pili:                 Tumeletwa hapa duniani kwa ajili ipi???
3          Tatu:                Nini khatima ya maisha yetu  ya duniani???

Jawabu ya suala la kwanza tunalipata katika Qur-an(95:4)
“Bila ya shaka tumemuumba Mwanaadamu kwa  umbo lilo bora  zaidi”.
Kumbe sisi ni wanaadamu  tumeumbwa kwa umbile lililo bora zaidi, na  ubora  wa umbile hilo unatokana na akili,fikra na mawazo tuliyopewa katika kuamuwa maamuzi yetu . Hivyo Mwanaadamu akitumia akili yake vizuri huongoka na akawa bora kuliko kiumbe chochote ulimwenguni na kinyume cha hivyo hupotoka na akawa chini ya walio chini kama aya inavyo tufahamisha (95:5). 
“Halafu tukamrudisha chini kuliko walio chini” 
 Vilevile ayya ya 30 ya surrat Baqarah inatufahamisha .
 “Wakumbushe watu khabari hii :Wakati MOLA wako alivyowambia Malaika “Mimi ninaleta viumbe wengine kukaa katika ardhi”(nao ndio wanaadamu) wakasema Malaika “utaweka watakaofanya uharibifu humo na kumwaga damu,  hali sisi tunakutukuza kwa sifa zako na utakatifu wako ?”Akasema (M/MUNGU) “Hakika mimi nayajua msiyo yajua”
Ayya hii inatufahamisha kuwa Mwanadamu hakuzuka tuu kwa bahati mbaya ,isipokuwa ameletwa na M?MUNGU Bwana wa viumbe vyote .
Jee, M/MUNGU ametuleta duniani bila ya malengo yoyote ?.
Jawabu ya suala la pili Qur-an (51:56)
“Sikuwaumba majini na watu ila wapate kuniabudu”.
Katika ayya hii M/MUNGU ametuwekea wazi lengo hasa la kuwepo kwetu duniani . Jawabu ya suala la tatu . Katika suala la khatima ya maisha yetu ya ulimwenguni ni kwamba : waislamu tunaamini tutakufa ,tutafufuliwa , tutakusanywa na tutahesabiwa (tutahukumiwa)(45:26)
Kwa yale tuloyatenda ulimwenguni .Kwa hakika maisha ya duniani ni mafupi na yakupita na maisha ya kweli yako huko akhera . Qur-an (87:16-17)
 “Lakini nyinyi mnayapenda maisha ya dunia . Hali yakuwa (maisha ) ya akhera ni bora na yenye kudumu”  .
Siku ya malipo watu watagawika sehemu mbili .Qur’an (79:37-41) “Ama yule aloasi Na akapenda zaidi maisha ya dunia .Basi kwa hakika jahannamu ndiyo itakayokuwa makazi yake ,Na ama yule aliyeogopa kusimamishwa mbele ya MOLA wake ,akaikataza nafsi yake na matamanio( maovu )Basi pepo ndiyo itakayokuwa makazi yake.
Nasifa za watu wa peponi tunazipata katika sura ya (56:15-37) “Watakaa juu ya viti vya faharii , kuelekeana kuzungumza ,na watakunywa vinywaji vya kila namna ,hawataumwa na vichwa wala kutokwa na akili , Watakula matunanda wayapendayo na nyama za ndege kama watakavyo tamani .Watapata W/ke wazuri wenye macho mazuri na makubwa  mithili ya lulu . Humo hawatasikia maneno ya upuuzi na  ya dhambi isipokuwa maneno ya salama na Amani .Watakuwa katika vivuli vya mikunazi isiyo na miba na migomba iliyopangiliwa pamoja na maji yanayominika .Na wake watukufu (waliokuwa nao duniani)wataumbwa kwa umbo bora zaid.Na M/MUNGU anamalizia kwa kusema  “Tutawafanya vijana kama kwamba ndio kwanza wanaolewa ,watapendana na waume zao waliohirimu moja.”.
Ama watu wa Motoni sifa zao(adhabu) zimetajwa katika sura mbali mbali kama vile sura ya 56,69,88 n.k , kwa ufupi hali itakuwa mbaya sana maana ni adhabu juu ya adhabu .M/MUNGU ataamrisha “Mtupeni motoni katika mnyororo wenye dhira sabini”chakula ni maji ya usaha na miba , watakuwa katika upepo wa maji ya chemkayo ,na kivuli cha moshi mweusi sana si chakuleta baridio wala starehe na kinywaji cha humo nimaji ya chemkayo .
Naturudi katika maada yetu ambayo tuihusisha moja kwa moja na jawabu ya suala la pili (51:56)
“Siku waumba majini na watu ila wapate kuniabudu”
 Huu ni wajibu wa Waislamu, lakini kabla kuangalia Suala zima lakuabudu ni lazima tujuwe maana ya dini “Dini ni mfumo wowote wa maisha anaofuata mwanaadamu katika kuendesha maisha yake ya kibinafsi na jamii kwa ujumla katika nyanja zote za maisha”
Sasa sisi waislam ambao tumeamuwa kufuata mfumo wa kiislamu ambao ndiyo mfumo wa haki “Bila ya shaka dini (ya haki ) mbele ya M/UNGU ni Uislam………”(). Hatuna budi kuufuata mfumo huo kikamilifu.
      enyi mlioamini !Ingieni katika hukumu za Uislam zote, wala msifuate nyayo za shetani , kwa hakika yeye kwenu ni adui dhahirii”. (2:208)
Suala linajitokeza , Vipi tutaweza kumuabudu  Allah (s.w)na kuuingia Uislam wote.
     Jawabu:- Elimu ndio zana pekee aliyotunukiwa Mwanaadamu ili aitumie katika kutekeleza wajibu wake.Naye Mtume(s.a.w) wahyi na amri ya kwanza aliyopewa na Mola wake ni kusoma kwa ajili ya Allah (s.w) Qur’ani (96:1-5).
Ni wazi kuwa Muislam mwenye tabia ya  kujielimisha katika mambo muhimu ya maisha kwa lengo la kupata ufanisi katika kumuabudu Allah(s.w) atatofautiana sana kiutendaji na kiuchaji na yule ambae hana sifa ya kujielimisha kama tunavyojifunza katika Qur’ani(39:9)
“…Je! Wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojuwa ?Wanaotanabahi ni  wale wenye akili tu.”  Vilevile (58:11) “…..Allah atawainua daraja wale walioamini miongoni mwenu na walio pewa elimu watapewa watapata daraja zaidi.” Pia “….Kwahakika wanaomuogopa Allah miongoni mwa waja wake ni wale wataalamu (waliosoma)”
Aya zilizopo hapo juu zinatuekea wazi dhana nzima ya kuabudu ,itafanikiwa ikiwa Waislam tutajifunza na kuifanyia kazi elimu tuliyonayo , ukizingatia maneno ya Mtume (s.a.w) “Kutafuta elimu ni faradhi kwa kila muislamu  MwanamumenaMwanamke.
Kwani madhara gani yatajitokeza endapo waislamu hawatakuwa na utamaduni wa kujisomea ?
Madhara makubwa yatajitokeza katika jamii ,kama tunavyoona katika jamii yetu ya Kizanzibar na Kiislam kwa jumla:-
1                  Waislamu kutoufanyia kazi Uislam wao .(hawaujui)
2                  Waislamu wengi wanabaki kuwa waislam majina tuu .
3                  Waislamu wanaona tabu (wanaona haya) kujitambulisha kuwa wao waislamu.
4                  Waislamu kufuata mila zisizokuwa za Kiislam.
5                  Kuutupa (kuugawa) Uislam na siasa (amakueweka tofauti na siasa)
6                  Uislam unashindwa kuwa juu ya dini zote kama kama Allah(s.w)alivyoahidi.
Kutokana na matatizo tuliyokwisha ya orodhesha hapo juu, ni dhahiri kuwa lengo la kuabudu halitofanikiwa, na hapo waislamu wanabaki na dhana ya kuwa Uislamu (au ibada),ni nguzo tano .Shahada, Swalaa,Zakah,Funga na Hijja.Hili ni wazo potofu.
 Mana haiwezekani M/Mungu kutuwambia kuwa lengo la kuumbwa kwetu ni kumuabudu katika maisha yetu yote alafu ibada yenyewe iwe :-
1     Swala tano (5) za faradhii ambazo tunatumia saa moja kuzisali katika masaa 24.
2     Zakah  ambayo hutolewa na Mtu mwenye uwezo katika kiwango na muda  maalum.
3     Funga ambayo tunafunga mwezi mmoja(1) katika miezi kumi na mbili (12).
4     Hijja ambayo hutekelezwa   na Mtu mwenye uwezo ,mwaka mara moja .
Ukweli utabaki palepale kuwa nguzo tano za Uislamu ni msingi wa ibada ,hivyo mafunzo yanayopatikana humo kupitia msingi huo ndio hasa yatakayokamilisha ujenzi wa nyumba  ya Uislam.
Swala: Humkataza mtu maovu na machafu yote . hivyo Waumini  hatuna budi kuachana na maovu na machafu yote .
Zakah : Humtakasa mja kutokana na mali yake, nafsi yake  na jamii kwa ujumla .
Funga:Funga humfanya muumini kuwa mcha mungu .
Hijja: Inatufunza Umoja na Usawaa pamoja na Utii kwa Allah (s.w) kubwa zaid ni dhana nzima ya kukumbushana mema na kukatazana mabaya funzo hili tunalipata katika Uwanja wa  Arafa.
        
Maafa makubwa yameikuta jamii ya Waislam wa  Kizanzibari  , ambapo hata tunashindwa hata kujielewa kuwa ni waumini au siwaumini wa dini ya Kiislamu. Mafundisho ,mila na desturi za kitwaghuti  tumezikumbatia na Uislam tumeupiga teke ,tumesahau wajibu wetu na sasa tunakufuru  ,shime Waislamu  turudi  kwa Mola wetu ,tufuate Qur’an na Sunna za Mtume wetu (s.a.w).Tuanzishe mashule ya Kiislamu ,yatakayofuata utamaduni wa Kiislamu kwa ajili yakutowa mafunzo Kiislamu .Ndugu zangu waislamu .Waislamu kutafuta elimu ndiyo roho ya Uislamu.Kukumbushana mema na kukatazana mabaya ndiyo chakula cha n! yoyo za Waislamu .Kufuata mafundisho ya Mtume (s.a.w) ndio mafanikio ya Waislamu .  Kumtumikia ,kumnyenyekea  na kumuabudu M/Mungu ndio wajibu wa Waislamu .
Qur’an (103:2-3)
“ Hakika binaadamu yuko katika hasara. Isipokuwa wale walioamini na Wakafanya vitendo vizuri wakausiana (kufuata)haki na wakausiana (kushikamana) na subira (kustahamiliana) .” YARABII TUJALIE NA SISI  KATIKA WALIOAMINI NA WENYE MAFANIKIO KATIKA HUKUMU YAKO .
AMIIIIEN .
WABILLAHI  TAWFIQ
Ndugu yenu SULEIMAN ABDALLAH katika njia ya kuamshana .

No comments:

Post a Comment